Rais mpya wa Iran ashika madaraka
 
Rais mteule wa Iran Hassan Rouhani anaapishwa katika sherehe mjini 
Tehran ambapo atapewa idhini ya kiongozi wa kidini nchini humo, 
Ayatollah Ali Khamenei. 
Rouhani ambaye alikuwa mpatanishi kwenye mazungumzo ya mradi wa 
nuklia wa Iran, alishinda uchaguzi wa urais nchini Iran katika duru ya 
kwanza.
                     
Wakati wa kampeni zake rais huyo mteule aliahidi
 kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, na alisema ataimarisha 
uhusiano kati ya taifa hilo na jamii ya kimataifa ambao uliharibika 
zaidi wakati wa utawala wa Rais Mahmoud Ahmedinejad.
SOURCE:BBC 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment