Dk Ndalichako ‘achanachana
             Arusha: Katibu Mtendaji wa Baraza la 
Mitihani Nchini (Necta), Dk Joyce Ndalichako amesema karatasi za majibu 
ambazo wamekuwa wakizipata kutoka kwa wanafunzi zinaonyesha kuwa, watoto
 wengi wanahudhuria shuleni lakini hakuna wanachojifunza.
 P.T
Arusha: Katibu Mtendaji wa Baraza la 
Mitihani Nchini (Necta), Dk Joyce Ndalichako amesema karatasi za majibu 
ambazo wamekuwa wakizipata kutoka kwa wanafunzi zinaonyesha kuwa, watoto
 wengi wanahudhuria shuleni lakini hakuna wanachojifunza.
 P.T
         
Dk Ndalichako aliyasema hayo jana 
jijini hapa alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa mabaraza ya mitihani
 ya Afrika, ambao umejikita kujadili suala la tathimini ya elimu kwa 
nchi za Afrika.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk 
Ndalichako kuzungumza tangu Serikali itangaze kufuta matokeo ya kidato 
cha nne mwaka 2012 na kutaka yapangwe upya, suala ambalo lilipingwa na 
wadau wengi wa elimu.
Alisema kuwa wakati nchi nyingi za 
bara hili zikiwa zimejitahidi kuongeza upatikanaji wa elimu kwa watu, 
ubora wa elimu unaendelea kuwa tishio kwa watu wa bara hili kwa vizazi 
vijavyo.
"Kama mabaraza ya mitihani, tumekuwa 
tukiona karatasi za majibu kutoka kwa wanafunzi ambazo zinaonyesha kwa 
uwazi kabisa kuwa watoto wanahudhuria shuleni lakini hakuna 
wanachojifunza," alisema Dk Ndalichako.
Kwa upande wake Profesa Justinian 
Galabawa, alisema ili kuendeleza elimu, lazima uamuzi wa kitaalamu 
usiingiliwe na siasa kwa namna yoyote ile.
Alitolea mfano kitendo cha Serikali kufuta matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2012 akisema hakikuwa sahihi hata kidogo.
Alisema lazima vyombo vilivyopewa 
mamlaka kisheria kama Necta viachwe vifanye kazi bila kuingiliwa kwani 
kufanya hivyo kutaporomosha elimu.
Alisema pia lazima kuwa na sera ya 
nchi ya kufanya tathmini ambayo ili ifanye kazi lazima ishirikishe wadau
 wote na kila anayehusika kuitekeleza awe nayo.
"Jambo la kwanza ni lazima tuheshimu 
wataalamu na wasiingiliwe na wanasiasa, taasisi zilizoundwa kisheria na 
kupewa mamlaka ya kupima na kutambua watu ni lazima ziheshimiwe. Kama 
mtoto amepata daraja la nne huwezi kumpa la kwanza," alisema Profesa 
Galabawa.
Kwa upande wake, Makamu wa Pili wa 
Rais wa Zanzibar, Seif Ali Iddi alisema mkutano huo ni sehemu nzuri ya 
Tanzania kujifunza kutoka kwenye nchi nyingine kujua ni nini watu 
wengine wanafanya.
Alisema uzoefu utakaopatikana kutokana na mkutano huu utasaidia katika kujipima na kuendeleza elimu nchini.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo, 
Philipo Mulugo alisema kwa siku ya kwanza tu wamebaini kuwa zaidi ya 
asilimia 80 ya nchi za Afrika tayari wanatumia mfumo wa usahihishaji kwa
 kutumia mashine maalumu (OMR) ambao bado baadhi ya watu nchini 
wanaulalamikia.
Alisema baadhi ya nchi sasa wameanza 
kusahihisha kwa kutumia kompyuta hata maswali ya kujieleza, hivyo 
akawataka Watanzania waache kujirudisha nyuma.
P.T
chanzo: mwananchi
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment