ANC kususia ibada ya Marikana
 
Maelfu ya raia wa Afrika Kusini wamekusanyika katika 
mgodi mkubwa wa dhahabu nyeupe kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuuawa kwa 
wachimba migozi 34. Chama tawala cha ANC kimesema hakitahudhuria 
makumbusho ya leo kikisenya yanatumiwa kukejeli utawala wa nchi.
                     
Katika maadhimisho hayo Afisa mtendaji wa 
kampuni ya, Lonmin, Ben Magara amwaomba mshamaha familia za wachimba 
migodi 34 waliouawa. 
                     
Tofauti kati ya makundi mawili ya 
vyama vya wafanyikazi zililaumiwa kwa kuzuka vurugu zilizotokea mwaka 
jana.Chama kilicho na uhusiano wa karibu na ANC- National Union Of 
Mineworkers kimepingwa na wachimba migodi wengi na kuanzisha chama 
kipya. Mauaji hayo yalisababisha gathabu ya umma na kupelekea lalama 
nyingi dhidi ya sekta ya madini.
                     
Afrika Kusini ina asili mia 80 ya madini ya 
dhahabu na dhahabu nyeupe.Mauaji ya wafanyikazi hao yalitajwa kuwa 
mabaya zaidi tangu kumalizika kwa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini mwaka 
1994. Sherehe za leo zimepangwa na chama kipya cha kutetea maslahi ya 
wachimba migodi Mineworkers and Construction Union (Amcu) ambacho 
kinashinikiza nyongeza zaidi ya marupurupu ya wafanyikazi.
                     
AMCU ndicho kikubwa zaidi katika mgodi wa 
dhahabu nyeupe inayomilikiwa na kampuni ya Lonmin.Baadhi katika chama 
tawala cha ANC wameelezea hofu huenda chama hicho kikaungana na aliyekua
 kiongozi wa vijana Julius Malema ambaye alifukuzwa chamani kwa makosa 
ya nidhamu.
                     
Malema ameunda chama chake cha kisiasa. Rais 
Jacob Zuma aliunda tume ya kuchuguza matukio yaliyopelekea mauaji ya 
wachimba migodi hio. Mwandishi wa BBC Afrika Kusini anasema kumekuwa na 
ghathabu ya umma kwani hadi sasa hakuna polisi hata mmoja 
aliyewajibishwa na mauaji hayo.
CHANZO:BBC 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment