Jeshi Nigeria "lamua" kamanda wa Boko Haram
 
Jeshi nchini Nigeria limetangaza kuwa limemua kiongozi wa ngazi ya juu wa kundi la Boko Haram.
                     
Taarifa hizo za kijeshi zemesema kuwa kiongozi 
huyo aliyeuwawa ni Momodu Bama,ambaye ni wa pili katika uongozi wa kundi
 hilo la wapiganaji.
Mapema mwezi huu wafuasi wengine wa 
kundi hilo la Boko Haram ambao walikuwa wamekamatwa walifichua kwamba 
huyo kamanda wao alikuwa ameuawawa.
                     
Msemaji wa Jeshi Brig Jenerali Chris Olukolade 
amesema Momodu Bama, ambaye pia anafahamika kama "Abu Saad", alikuwa na 
ujuzi wa kufyatua makombora ya kutungua ndege.
                     
Mapema mwezi wa Mei, Nigeria ilitangaza hali ya 
hatari katika maeneo ya kaskazini Mashariki mwa nchi ili kupambana na 
wapiganaji wa Boko Haram.
                     
Hata hivyo hadi sasa hakuna taarifa huru 
kuthibitisha kuuwawa kwa Bwana Momodu Bama nao Boko Haram wenyewe hawaja
 thibitisha kifo cha kiongozi huyo.
                     
Jenerali Olukolade, alisema Momodu Bama alikuwa 
ni mmoja ya viongozi wa Boko Haram waliokuwa wakitafutwa zaidi na 
kulikuwa kuna zawadi ya dola $155,000, £100,000 kwa yeyote atakaye toa 
habari zitakazosaidia kukamatwa au kuuwawa kwake.
CHANZO:BBC 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment