Clinton ampongeza Rais Paul Kagame
Aliyekuwa rais wa marekani Bill Clinton amempongeza 
rais wa Rwanda Paul Kagame licha ya madai kwamba amekuwa akiunga mkono 
makundi ya waasi katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo 
yanakiuka haki za kibinadamu.
                     
Bwana Clinton amesema katika mahojiano na BBC kwamba madai hayo ambayo Rwanda inayakataa hayajathibitishwa mahakamani.
                     
Pia alisema kuwa kuna changamoto kubwa katika 
mpaka wa Rwanda na Congo, kwani una watu chungu nzima ambao walihusika 
na mauaji ya halaiki miaka ya tisini.
                     
Lakini bwana Clinton amesema kuwa anathamini 
serikali ya Rwanda kutokana na mafanikio ya kiuchumi yalioafikiwa chini 
ya rais Kagame.
                     
Kiongozi huyo amekuwa akizuru mataifa ya Afrika pamoja na mwanawe Chelsea ili kujionea miradi ya wakfu wake.
SOURCE:BBC 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment