ABUNUWASI KAMA KADHI 
Abunuwasi alikuwa mshairi maarufu katika mahakama ya khalifa Haruni 
Rashidi. Siku moja Khalifa alimteua Abunuwasi kuwa Kadhi mkuu wa jiji,  
Asubuhi moja mpishi wa keki akaenda kuonana na Kadhi na kulalamika 
kuhusu bwana mmoja masikini. Mpishi analalamika: 'huyu ombaomba 
anasimama tuu karibu ya kibanda changu pale sokoni ninapo oka keki zangu
 tamu. ananusa tuu harufu nzuri bila kunilipa, kwahiyo mimi ninakuwa 
nikifanya kazi bure.'
Abunuwasi kama Kadhi mwenye busara akalifikiria swala hili kwa muda 
kidogo, kisha akatoa hukumu: akamwambia mpishi ''unachosema ni kweli 
kabisa. huyu ombaomba amefaidi harufu ya keki zako na kwa kufanya hivyo 
ametumia matunda ya kazi yako. Kwa hilo itabidi akulipe fidia. Nafikiri 
dinari mbili za dhahabu zitakuwa ni fidia inayofaa kabisa.'' Macho 
yampishi yakang'aa aliposikia dinari mbili, lakini masikini akalalamika:
 "Mungu mkubwa, mimi ni masikini, sina pesa, hata ukinitingisha 
hutasikia mlio wa njuga. Unaweza ukakamua maji ya matunda kwenye zabibu 
lililo kauka? Abunuwasi akalifikiria tena hili kwa muda alafu akasema: 
ikiwa wewe ni masikini, nitakulipia hii fidia toka mfukoni kwangu.' 
Abunuwasi akatoa sarafu mbili, mpishi akanyoosha mkono wake  wa kulia 
kwa shauku kubwa ili apokee fidia yake.
Mara moja Abunuwasi akabadilika na kuanza kumuhoji  mpishi, 
Abunuwasi: Je huyu masikini alikula keki zako?
Mpishi: Hapana Mkuu
Abunuwasi: Je alizinyofoa?
Mpishi: Hapana Mkuu
Abunuwasi: Labda aliziharibu kwa kuzipumulia?
Mpishi: eeh, Hapana Mkuu
Abunuwasi: Kwa hiyo unaweza ukaziuza ama umeshaziuza?
Mpishi: Ndio Mkuu ninaweza nikaendelea kuziuza na zingine nimeshauza
Abunuwasi: Kwa hiyo basi kama huyu bwana hajala, hajanyofoa wala 
kuzipumulia keki zako, zaidi ya kuvuta harufu nawe basi utafidiwa na 
sauti. fungua masikio yako kwa makini ili nawe ufurahie sauti za dinari 
mbili za dhahabu. ikabidi mpishi afanye hivyo kwa sababu hii ndio 
ilikuwa fidia pekee ambayo angeweza kupata
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment