Thursday 18 July 2013

KISOMO KWANZA



              
1 Masomo kisha kuanza,
Busara ni kujifunza,
       Jisomee,
       Usizembee,
       Uzingatie,
Pole pole utaweza.

2.     Mwalimu kwako hazina,
Yakichwani kwake vuna,
       Sifanye dhihaka,
       Mandiko andika,
       Nidhamu weka,
Tafika pasi na shaka.

3.   Hudhuria masomoni,
Sikimbie mitihani,
       Waogofya nini,
       Hakuna mageni,
       Ni yadarasani,
Haraka rudi kundini.

4.   Mitandao isikughiribu,
Kisomo kuona tabu,
       Si facebook,
       Si twiter,
       Si you tube,
       Elimu ni wako mtabibu.



  
5.   Acha kukodi sidii,
Kisomo ongeza bidii,
       Fanya,
       Diskasheni,
       Pamoja unganikeni,
Si budi kupata wani.

6.     Maneno mengi huchosha,
Mwanafunzi nakwamsha,
       Nia anza,
       Kisomo kwanza,
       Kichwani tunza,
Elimu ndio maisha.

DEOGRATIAS MMUYA
S.L.P 2197
DODOMA
Phone no 0763757782/0653602460

No comments:

Post a Comment