Monday 29 July 2013

SABABU ZA YANGA KUGOMEA KUONYESHWA MECHI ZAKE ZA LIGI KUU MSIMU UJAO NA AZAM TV NI HIZ HAPA
















Uongozi wa klabu ya Yanga leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu ya urushwaji wa michezo yake ya Ligi Kuu katika kituo cha luninga cha Azam ambacho kimeingia makubaliano na kamati ya Ligi Kuu  kuonyeshwa michezo yote ya ligi kwa kipindi cha miaka miatatu (3).
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa klabu ya Yanga Yusuf Manji amesema uamuzi wa kamati ya ligi kuingia mkataba na kituo cha Azam Tv bila ya kuwashirikisha wahusika wenyewe ambao ni vilabu vishiriki haukuwa sawa.
Sisi kama klabu ya Yanga tulikaa kikao cha kamati ya utendaji na kuona taratibu za kupewa haki ya matangazo kwa kampuni ya Azam haikua sawa, sisi viongozi wa kalbu ya Yanga hatukushirikishwa katika mchakato huo hivyo tukaona ni vema tuje kwa vyombo vya habari tuulezee umma juu ya maazimio ya kamati ya utendaji.
Ifuatayo ni taarifa kamili kwa vyombo vya habari: 
YAH: URUSHWAJI KATIKA TELEVISHENI MICHEZO YA YANGA.

Hivi karibuni, Tanzania Football Federation (TFF)  iliunda Tanzania Premier League chini ya Bodi ya mpito Bodi ya TPL ambayo ni msimamizi mpaka hapo Bodi itakayokuwa imechaguliwa kidemokrasia. Bodi hii imeamua peke yake kuingia katika mkataba wa miaka 3 (mitatu) na kampuni inayoitwa Azam Television (ambayo ina  mapromota wale wale wanaomiliki Azam Football Club). Makubaliano ambayo Bodi ya TPL inatarajia kuingia na Azam Television, Kamati ya Utendaji ya YANGA inalipinga kwa nguvu zote katika misingi ifuatayo:

1. BODI YA TPL

1.1 Bodi iliyoko sasa hivi ni ya mpito ambayo ilitakiwa kutenguliwa na Bodi iliyochaguliwa kidemokrasia kwa kupitia uchaguzi wa tarehe  ……….. mwaka huu na haitakiwi kuingia katika mikataba a miaka mingi wakati inakaribia kuondoka katika ofisi.

1.2 Bodi ya TPL iliyoko sasa hivi haikuchaguliwa kidemokrasia.

1.3 Bodi ya TPL iliyoko sasa hivi haina mjumbe hata mmoja aliyeteuliwa kutoka YANGA.

2. UTARATIBU WA DUNIA NZIMA

2.1 Haijawahi kutokea katika ligi ya mpira wa miguu ya kisasa kulazimishwa kwa Klabu inayoshindana katika ligi kuachia haki zake za urushwaji wa michezo zichukuliwe na chombo cha habari cha Klabu ya upinzani. 

2.2 Mfumo (undertaking) ambao TPL inataka kuanzisha kwa njia ya kulazimisha mkataba kwa YANGA iachie  urushwaji wa michezo yake ya soka yarushwe na Azam TV unatishia sana uwepo wa msingi wa ushindani katika soka ya Tanzania.

2.3 Makubalianokati ya TPL na Azam Television kuhusu utaratibu wa malipo yanasemakwamba Klabu ya YANGA na Klabu zingine zitakazoshiriki katika Ligi Kuu ya Tanzania  watapata mgao sawa wa mapato ya urushwaji wa michezo hii, ambayo YANGA inapinga kwa sababu kama inavyofanyika duniani kote kwenye ligi zilizofanikiwa (angalau) kutofautisha mgawanyo wa mapato kati ya timu kufuatana na matokeo ya mwisho wa ligi.

2.4 Kamati ya Utendaji ya YANGA siyo tu haikubaliani na mgawanyo sawa wa mapato ambao hautofautishi kati ya timu ya kwanza katika ligi na timu ya mwisho katika ligi, lakini pia ukosefu wa viwango (premiums) vitakavyolipwa: 

2.4.1 Vilabu vya mpira vyenye ufuasi wa washabiki wengi; 

2.4.2 Vilabu vya mpira vinavyoendeshwa na Wanachama; 

2.4.3 Vilabu vya mpira visivyopata ruzuku kutoka Serikalini n.k.

3. MIGOGORO YA MASLAHI

3.1 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mpito ya TPL ni Mkurugenzi mwandamizi wa Makampuni ya Azam na  kwa hivyo mazungumzo ya siri kati ya Bodi ya TPL na Azam ni ya kutiliwa mashaka.

3.2 Makampuni ya Azam yana yanashindana kibiashara na makapuni mengi yakiwemo ya utengenezaji wa vinywaji baridi na imeonyesha huko awali inaweka “matakwa maalum” muhimu zaidi kuliko mprira  wa miguu, kama vile Azam F.C. hawashiriki katika Kombe la Tusker na kwa hiyo YANGA inakuwa na msimamo kwamba kwa Azam Television kupewa leseni ya kurusha matangazo ya mpira wa miguu inatishia biashara za washiriki wa sasa na wa baadaye wa YANGA.

3.3 Azam na YANGA wana uadui wa kimichezo. Kumbuka, wakati MRISHO NGASSA alipotaka kwenda YANGA, Azam F.C. walimkopesha kwa nguvu kwa Klabu ya Simba! Kwa hiyo YANGA itahatarika kwa matangazo yenye upendeleo kama Azam Television itarusha hewani michezo yake n.k.

4. KUTOKUWA NA UWAZI

4.1 Mkataba wa utangazaji wa miaka mingi unaotaka kuingiwa kati ya TPL na ambao badohaujarushwa Television ya Azam haukushindanishwa na vyombo vingi vya habari,  na vyombo ambayo wako tayari kwenye soka havikujulishwa kuhusu fursa hii au walizuiliwa kufikisha mapendekezo yao ya maombi ya haki za kurusha matangazo katika Ligi Kuu (Tanzania Premier League).

4.2 Ukosefu wa uwazi wa TPL unanonyesha kuwa MoU iliyokusudiwa kuwekewa saini na TPL haikufikishwa YANGA kwa ajili ya mapitio ya kisheria, licha ya YANGA kufanya ombi hilo kwaTPL.

5. MAZINGATIO YA KIBIASHARA 

5.1 Mamlaka ya kuamua mzozo wowote wa mkataba wa leseni ya utangazaji wa Ligi Kuu (Tanzania Premier Leagu) itakuwa ni Mahakama ya kisheria na siyo FIFA. TPL inasingizia  kwamba leseni ya matangazo ambayo inakusudia kufanya kuwa ni maagizo ya FIFA na kwa hiyo YANGA inapaswa kuukubali "lock, stock and barrel."

5.2 TPL inaelezea kimakosa makubaliano ya leseni ya urushaji  wa mchezo ya mpira inayotarajia kuingia na Television ya Azam kama "makubaliano ya udhamini" (“sponsorship agreement”) ambayo siyo sahihi, kwa sababu urushaji wa michezo ya mpira wa miguu ni biashara inayotokana na maslahi ya uhusiano na hivyo 
wahusika wote ni lazima wazingatie maslahi yao ya kifedha.

Kwa mfano, moja ya vyanzo muhimu vya mapato ya YANGA ni mapato ya kiingilio ya mlangoni yatokanayo na michezo ya mpira wa miguu ambayo urushwaji wa michezo hii itapunguza mapato haya. Kwa wastani michezo ya YANGA  Dar es Salaam huingiza makusanyo ya mlangoni shilingi milioni 50 kwa kila mchezo na hata kushuka kidogo kwa 25% katika mahudhurio ya mechi za YANGA zinafikia mara mbili ya mapendekezo ya mapato takribani Sh milioni 8.3 kwa mwezi kupokelewa na YANGA kutoka mradi wa kibiashara kati ya TPL na Azam Television. Kwa kuzingatia haya, kwamba hata siku za nyuma kama kulikutokea fursa ya kurusha mchuano wa mpira unapochezwa, wadau wote (Timu za mpira wa miguu, TFF na Mtangazaji)  walikuwa wanaafikiana kwanza kwa pamoja kuhusu mapato na mgawanyo wake.

Kamati ya Utendaji ya YANGA ina maoni kwamba makubaliano yoyote ya kibiashara yanayoihusu ni lazima iyalinde maslahi kifendha ya Klabu yake ambapo makubaliano ya TPL / Azam Television hayaangalii na kwa hiyo, Kamati ya Utendaji ya YANGA haitaki mchezo wake urushwe hewani na Azam Television.

Msisitizo wa TPL kuwa lazima Azam Television irushe hewani michezo ya YANGA linasikitisha. Kamati ya Utendaji ya YANGA haina tatizo na Vilabu vingine vya mpira wa miguu zikiruhusu michezo yao kurushwa na Azam Television ila haifurahii kuwa TPL inalazimisha YANGA kuonyesha mchezo wake wa Vodacom Premier League katika Azam Television.
......................
(YUSUF MANJI)
MWENYEKITI
YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB
29 JULAI, 2013

Naibu Waziri Tizeba atishia kumuua Kaka yake, Kisa tofauti za Kisiasa

UGOMVI wa kisiasa kati ya ndugu wawili wa familia moja, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba(ccm) na kaka yake Adrian Tizeba(Chadema) umechukua sura mpya baada ya kutishiana kifo.

Akizungumza na gazeti hili jana, Adrian alisema kuwa tangu ahame CCM na kujiunga na CHADEMA, mdogo wake huyo amekuwa akimbambikizia maneno mabaya yaliyoleta uhusiano mbaya katika familia yao.

Alidai kuwa naibu waziri huyo aliwahi kumwambia mama yao mzazi aseme kwamba Adrian aliwahi kumbaka.

Alisema kuwa hayo yote yanasemwa ili afunguliwe mashtaka na kufungwa.

Adrian aliongeza kuwa baada ya uchaguzi mdogo wa madiwani katika ya kata ya Lugata ambapo naibu waziri huyo alimtumia mama yake kuendesha propaganda chafu dhidi yake, sasa amebambikiziwa tuhuma mpya.

Alisema baada ya uchaguzi huo alibakia katika kata hiyo iliyo kisiwani kwa lengo la kuendelea na kazi za kisiasa, lakini naibu waziri amembambikizia kesi kuwa anazuia mgambo kufanyika katika eneo hilo.

Hali hiyo imesababisha polisi na wanajeshi kumsaka kwa nguvu ikiwemo kumtengenezea shtaka la wizi wa kutumia silaha.

Alifafanua kuwa siku za karibuni kwenye kata hiyo kumekuwa na kitendo cha kulazimisha vijana kushiriki mgambo bila hiari yao.

Alisema kuwa katika kutengeneza sababu ya kuwabana, polisi walitumia vurugu za tukio la kijana Emanuel Joseph kunyang’anywa baiskeli yake na wakufunzi wa mgambo wakidai kuwa vijana walimpiga mkufunzi na kuchaniwa sare za jeshi.

Alipotafutwa Naibu Waziri Tizeba kujibu tuhuma hizo za kutishia kumuua kaka yake alisema hayo ni masuala ya familia ambayo hayana nafasi ya kuandikwa katika vyombo vya habari.

“Ninashangaa kila kunapotokea kutoelewana kati yetu huyu kaka yangu anakimbilia kwenye vyombo vya habari wala sio kwenye familia wakati bado tunaye mama yetu mzazi ambaye anaujua vema mgogoro wetu.

“Mimi naona anafanya hayo akidhani kuwa angeweza kuniua mimi kisiasa lakini suala hilo halitawezekana,” alisema Tizeba.

Source: Tz Daima.

Pope slams gay lobby, wants bigger role for women

 

Pope Francis, fresh from a trip to Brazil, said on Monday he did not judge homosexuals but condemned the gay lobby as a "serious problem".

He also said women should be given a bigger role in the Church, but refused to consider their ordination, saying the "door is closed" on the issue.

Referring to homosexuals, the pope told journalists on the plane back to Rome: "The problem is not having this orientation, it is lobbying. That's the most serious problem I think."

"If someone is gay and seeks the Lord with good will, who am I to judge?"

Francis had to field questions about Battista Ricca, who was appointed by the pontiff to a key position at the troubled Vatican bank, but is embroiled in allegations that he had gay relationships with male prostitutes.

The pope said he had ordered a "brief investigation but we found nothing on him".

"I have not seen anyone at the Vatican who is registered as gay on his identity card. We acknowledge that there are (gays)," he said.

Nevertheless, "the catechism of the Catholic Church says clearly that we must not marginalise these people who should be integrated in the society."

The pontiff also gave a firm answer to a question on gay marriage and abortion -- both of which the Church opposes -- saying "you know perfectly the position of the Church".

The pope admitted in June that there is a "gay lobby" in the Vatican's secretive administration, the Roman Curia, according to a Latin American Catholic website.

SOURCE:AFP

"NIPO TAYARI KUJIUZULU ENDAPO ITABAINIKA NAUZA MADAWA YA KULEVYA'.....MBUNGE WA CCM (AZZAN) AFUNGUKA


MBUNGE wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan, amesema yupo tayari kujiuzulu ubunge, ikiwa itabainika anajihusisha biashara ya dawa za kulevya. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya kutajwa katika moja ya barua iliyosambazwa katika mitandao ya kijamii, baada ya mtu anayedaiwa kukamatwa China na kuwatuhumu watu kadhaa akiwamo Idd Azzan.

Akizungumza na MTANZANIA jana kuhusu sakata hilo, alisema hatua ya kuhusishwa na biashara haramu ya dawa za kulevya, ni kutotenda haki mbele ya jamii hasa wapiga kura wake na Taifa kwa ujumla.

Alisema mtu aliyendika barua ya tuhuma dhidi yake, ni wazi amedhamiria kumshushia heshima na huenda akawa ana jambo limejificha.

“Ni kweli nimeiona hiyo barua katika mtandao, inayodaiwa imeandikwa na kijana ambaye amekamatwa Hong Kong nchini China. Lakini ninajiuliza kama kweli yeye ni raia mwema, katika hili kwanini hakutaka kutaja jina lake kwenye barua hiyo.

“Hata nilipoisoma nimebaini kuwa huyo mtu ametumika na huenda kabisa hayupo nje ya nchi, kwani katika maelezo yake anataja jina la Balozi Philip Marmo kuwa amemsaidia hali ya kuwa hivi karibuni Rais Kikwete alimteua Balozi mpya Abdulrahman Shimbo na Marmo kuwa Balozi wa Shirikisho la Ujerumani.

“Kingine naona alijaribu kuandika uongo kuweza kuaminisha jamii, kwani hata hilo jila la balozi mwanzo limetajwa jina la Bernad na kukatwa kwa wino. Ninapenda kulieleza Taifa kuwa naomba vyombo vya usalama vifanye uchunguzi wa jambo hili na nikibainika ninauza dawa za kulevya nipo tayari kujiuzulu ubunge wangu.

“Kubwa haki itendeke katika kufanya uchunguzi wa jambo hili, ila ni lazima jamii na Watanzania kwa ujumla tusikubali kwa makusudi watu waichafue nchi yetu kwa chuki na fitna tu,” alisema Azzan.

Alisema kutokana na hali hiyo, anashindwa kuchukua hatua yoyote ya kufanya zaidi ya kuliandikia barua Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi dhidi ya barua hiyo kuweza kubaini ukweli wa jambo hilo.

“Sijawahi kuuza dawa za kulevya na hata katika familia yangu hakuna mtu anayefanya biashara hiyo haramu. Kila mmoja anajua kuwa Idd nilikuwa Diwani wa Kata ya Magomeni, huku kazi yangu kubwa ikiwa ni biashara ya magari na daladala ambayo ninaendelea nayo hadi sasa mbali ya ubunge kama nilivyopewa heshima na wapiga kura wangu wa Kinondoni,” alisema Azzan.

MTANZANIA ilipomuuliza kuwa ni hatua gani ikibainika hakuna ukweli wa jambo hilo baada ya vyombo vya usalama kufanya uchunguzi, alisema atakachokifanya anamuachia Mungu.

“Ni ngumu kusema hatua gani nitachukua ikibainika hakuna ukweli, lakini nataka kusema kama yule aliyeandika barua hii angetaja jina lake ni wazi baada ya uchunguzi ningeweza kuomba ushauri kwa mwanasheria wangu hatua za kuchukua, lakini kwa kuwa hakutaja jina ni ngumu kuweza kuamua,” alisema Azzan.

Kwa mujibu wa taarifa zilitolewa kupitia mitandao, ziliripoti kukamatwa kwa Watanzania wawili nchini China wakiwa na dawa za kulevya zenye thamani ya Dola milioni 3.34 za Marekani.

Chanzo: Mtanzania.

Ushindi wa kwanza Hamilton kwa Mercedes.

 

Dereva wa magari ya Timu ya Mecedes Lewis Hamilton ameweza kuishindia timu yake ushindi wake binafsi wa kwanza kwa Mercedes kwa kuongoza tangu mwanzo na kuwazidia madereva wenzake kwenye mashindano ya Hungary ya mbio za magari ya Langalanga au Formula 1.

Hamilton alijituliza na kutumia kasi akiwashinda dereva Kimi Raikkonen wa Timu ya magari ya Lotus aliyemaliza wa pili na Sebastien Vettel wa Red Bull aliyemaliza wa tatu.

Mark Webber wa Red Bull alionyesha umahiri wake kwa kujikwamua kutoka nafasi ya kumi alikoanzia mashindano hadi kumpiku dereva moto moto wa Timu ya magari ya Ferrari, Fernando Alonso.

Kutokana na hali hio Raikkonen sasa anapanda kwa pointi moja mbele ya Alonso akishika nafasi ya pili kwa jumla ya pointi alizokusanya tangu kuanza kwa mashindano ya msimu huu wa 2013/2014 ingawa bado yuko nyuma ya kiongozi wa mashindano na mtetezi wa taji Sebastien Vettel kwa pointi 38.

Kwa kipindi kirefu cha mashindano haya Fernando Alonso alikua katika jitihada za kuzuia asipitwe na Romain Grosjean wa timu ya Mercedes, na katika pilikapilika Romain Grosjean, alijitia matatani na kuadhibiwa kwa kupita gari akizunguka nje ya uwanja.

Wakati huo alimpita Felipe Massa wa Ferrari kwenye mzunguko wa 29 kituo cha nne, ambapo tairi zote nne zilivuka msitari mweupe unaobainisha uwanja na papo hapo kupewa adhabu ya kuuzunguka uwanja.

Hapo jana baada ya Hamilton kushinda nafasi ya mbele ya kuongoza mbio za leo alisema kua utakua muujiza endapo atashinda ikizingatiwa hali ya joto kali nchini Hungary bila kusahau matatizo yaloikumba timu ya magari ya Mercedes kwa matairi kupasuka kila mara.

Lakini alidhibiti mashindano kwa mda wote akipoteza uongozi kwa Grosjean na baadaye Mark Webber aliposimama kubadili tairi na mafuta lakini aliweza kurudi kileleni pale Webber aliposimama kubadili tairi na mafuta.

Kampeini zaelekea kileleni Zimbabwe

  
Rais mstaafu wa Nigeria Olesegun Obasanjo yuko 
nchini Zimbabwe kama mwangalizi wa uchaguzi mkuu

Kampeini za kisiasa nchini Zimbabwe zinamalizika hii leo kabla ya uchaguzi mkuu hapo Jumatano wiki hii.

Kiongozi wa chama cha Movement for Democratic Change ambaye pia ni Waziri MKuu ,Morgan Tsvangirai, hii leo atahutubia mkutano wa hadhara mjini Harare katika uwanja alikofanya mkutano wake hio jana Rais Robert Mugabe.

Viongozi hao wawili wamekua katika serikali ya muungano tangu mwaka wa 2008 na wametofautiana kuhusu muda uliowekwa kufanyika uchaguzi. Kumekua pia na madai ya wizi wa kura, na vitisho dhidi ya wafuasi wa MDC.

Shirika la kimataifa linalotathmini hali ya mizozo The International Crisis Group limeonya kwamba hakuna mazingira ya uchaguzi huru na haki Zimbabwe.

BBC

NANDO AMEIANGUSHA TANZANIA


Kama ilivyokuwa kwa Watanzania wengi, usiku wa jana ulikuwa mgumu sana kwangu. Mara nyingi nimekuwa nikiwashangaa mashabiki wa soka wanavyojikuta kwenye huzuni kubwa baada ya timu yao kufungwa.
Wengine hukosa hata hamu ya kula kwa siku kadhaa. Kwakuwa mimi si shabiki wa mpira, sijawahi kupata hisia hii. Lakini hatua ya jana usiku ya Biggie, kumchinjia baharini mwakilishi wa Tanzania wa Big Brother Africa, Ammy Nando aliyekuwa akitegemewa na wengi kuwa mmoja washiriki wanaoweza kuwa washindi wa mwaka huu, ilinifanya nihisi hisia kama wapatazo mashabiki wa soka, huzuni. Ni sababu iliyonifanya jana nilale mapema.

Nando aliondolewa (disqualified) kwenye shindano hilo kwa kuonesha utovu wa nidhamu, kumshambalia na kumtukana mshiriki mwenzie Elikem, na kumtishia maisha.

Ni kweli Nando alistahili adhabu ile na kwa kiasi kikubwa, ametuangusha sana. Japokuwa bado tuna matumaini kwa Feza Kessy, lakini kuondoka kwa Nando kumeiondoa hamu ya si tu Watanzania kufuatilia shindano hilo, bali kwa mashabiki wengi wa nchi nyingi za Afrika waliokuwa wanampenda Nando.

Mbaya zaidi ameondoka kwa sifa mbaya, uhuni, ujana wa kijinga, utoto, usela ma*i, ulimbukeni na hasira za mkizi. Nando alikuwa amebakiza wiki chache tu kufika kwenye mstari wa mwisho wa shindano hilo na huenda maisha yake yangebadilika milele kwakuwa alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda.

Alichokifanya Nando ni sawa na mwanafunzi aliyebakiza wiki mbili afanye mtihani wa taifa halafu anamtukana mkuu wa shule/chuo, usela ma*i haswaaa.

Nando alisahau kuwa ule ni mchezo na hauhusiani kabisa na maisha ya nje. Huenda hakupata muda wa kuzipitia vizuri sheria za shindano hilo, labda asingejiingiza kwenye fujo na uhuni wa aina ile.

Siku zake nzuri na za kuvutia kwenye jumba hilo, zimeharibiwa na dakika chache zilizotiwa dosari na mdomo wake na maamuzi ya kitoto ya kujifanya John Cena ama Floyd ‘Money’ Mayweather.

Uamuzi wa kumpa kibuti Nando, ulichukuliwa na Big Brother kufuatia ugomvi uliozuka Ijumaa hii kati yake na Elikem.
Bahati mbaya ni kuwa Nando ndiye aliyeuanzisha ugomvi huo na hivyo kumfanya avunje baadhi ya sheria za Big Brother.

“Any Housemate who becomes physically violent will be removed from the House immediately. Violence can refer to self-inflicted violence, or violence towards another. Violence includes provocation, goading, bullying and victimisation,” alisema Biggie.

Lakini katika msimu huu, Big Brother alianzisha sheria iliyopewa jina ‘Three Strike Rule’ ambayo itatumika kwa mshiriki atakayefanya kitendo kikubwa cha kuvunja sheria za shindano hilo.

Kutokana na ugomvi huo, Nando alipata Strike yake ya pili huku Elikem akipata moja.

Baada ya hapo, Nando aliitwa kwenye Diary Room na kupewa Strike ya tatu kwa kutishia maisha ya Elikem kwa kusema: “I feel like stabbing him. A nigga like that deserves to die”, (Najiskia kumchoka kisu. Mtu kama huyo anastahili kufa)
Mbaya zaidi ni kuwa, Nando alikutwa akiwa amelala na mkasi chini ya kitanda na hiyo si mara ya kwanza kukutwa akiwa na silaha kwenye jumba hilo. Ni wazi uwepo wa Nando kwenye BBA ulikuwa tishio kwa maisha yaw engine, ni kweli alistahili kutolewa ili kuepusha shari.
Mwezi uliopita alipata Strike ya kwanza na onyo kali kutoka kwa Big Brother baada ya kwenda na kisu kwenye party ya Channel O. Kisu cha nini sehemu kama hiyo? Nando bhanaa.

Umiliki wa silaha ama kusudi la kufanya ukatili kwenye jumba hilo ni kinyume na sheria za Big Brother.
Baada ya Diary session Nando jana, Nando aliambiwa afungashe virago mara moja huku pia Big Brother akitoa onyo kwa washiriki wengine kuishi kwenye jumba hilo kama watu wazima.

Biggie alikuwa na maana kubwa kuwaambia washiriki waliosalia ‘kubehave kama watu wazima’ kwakuwa tabia aliyoionesha Nando ni ya utoto uliopitiliza. Ana miaka mingapi vile?

Itawachukua muda mrefu Watanzania waliokuwa nyuma yake kumsamehe kwa ujinga alioufanya.

Bado haijulikani kama Nando anakuja Tanzania moja kwa moja ama ataenda Marekani alikokuwa akiishi. Kama atachagua kuja kwanza Tanzania, basi ategemee mapokezi hafifu kwakuwa amezivunja roho za watu wengi waliokuwa wakimpenda.

Nando atakuwa na wakati mgumu sana akija kuendelea na maisha ya kawaida kwakuwa amezingua kwa namna nyingi.Usisahau kuwa ana wakati mgumu pia kwa watu wa Ghana kwakuwa atatakiwa kusawazisha scandal yake na aliyekuwa mshiriki wa nchi hiyo, Selly ambaye anamtuhumu kuwa alimwambukiza STD. Kiufupi Nando ni adui mkubwa wa Ghana kwa sasa.

Selly anadai kuwa hakufanya mapenzi na Nando na mama yake amepanga kumshitaki Nando kwa kuchafua jina la bintiye, na ameshawasiliana na watayarishaji wa shindano hilo. Anasema ameshapimwa na wala hana ugonjwa wowote wa ngono na kwamba hajui Nando aliupata wapi ugonjwa huo.

Tusubiri kuona maisha mapya ya Nando akirudi mtaani. Pamoja na kutoka kwa aibu, bado atakuwa na future nzuri kwenye fashion industry barani Afrika na hata kwenye filamu, hasa zile za action!! Lol.

Hizi ni baadhi ya reactions za watu mbalimbali baada ya Nando kuondolewa kwenye shindano hilo.

Jocelyne Maro

If he had stayed composed he definitely would have won…what a wrong way to leave the house…shame…

$un$hine☀

Nando was a weak chap! U don’t brag about stabbing people n think thats strength. Be gone gangsta wannabe Tanzanian #BBATheChase

Godfrey Rugambwa

Nando umetuvua nguo watanzania mbele ya waafrika wote bro! Sasa nchi zote za Afrika zimeelewa kuwa hivyo ndivyo watanzania tulivyo! SAD. Namuangalia Bimp anakusanya kila kilichokuwa cha Kaka yetu (Nando) huku akiwa anahema vibaya sana! The dude is so damn cool All the best bro

KW ‏@keezywear

Nilikuwa naamini Nando angechukua 300 USD za #BBATheChase, but I was wrong… Ungeacha uhuni wako kwa siku chache zilizobaki Nando!!!

Hakeem Mandaza

Nandoooooo…… :( :( :( not happy

Christine Sintah

Kwanza Biggie kamuhurumia Nando kuanzia ijumaa mpake leo, hasira hasara , bambii Bimp

SebaTheWarrior: u cant threaten somebody’s life and expect people to treat u the same the next day..that’s how the cooky crumbles

♥ FEZA ♥ NANDO ‏@HPhillipo

Biggie jamanii why plsss why biggie whyyy ooooh! NandooooOoooo ☹#BBATheChase

jacqueline ulotu

Shame Tanzania.. Nando disqualified from the game.. #BBATheChase

Source:Bongo 5

Sunday 28 July 2013

We will get new players in, vows Moyes

 

Manchester United manager David Moyes said Sunday he was confident of getting new players in before the end of the transfer window and was mulling a third bid for Cesc Fabregas.

Barcelona have turned down two bids -- the latest reportedly of more than £30 million ($38 million) -- from United for the Spanish midfielder, 26, and new Barca boss Gerardo Martino on Friday insisted he was not for sale.

"I couldn't tell you at the moment and can't tell you if there will be another bid. Obviously we will take stock of it and consider what we are going to do next," Moyes said in Hong Kong, ahead of his side's friendly on Monday against local side Kitchee.

"What we've got here is a really good squad of players already, so you mustn't forget about the quality that is already here at Manchester United.

"Undoubtedly we are hoping to add to it (the squad) and I am confident we will do, certainly before the (transfer) window shuts.

On the so-far failed Fabregas bid he added: "I never at any time said I knew we would get (Fabregas), just that we had made offers that had been rejected. We'll take stock of the situation and see where we go from there."

The United boss, who has only been in the Old Trafford hot seat for four weeks, was tight-lipped about the future of striker Wayne Rooney, who has asked to leave the club and is currently injured.

Rooney is on schedule to return for a friendly in Stockholm on August 6, said Moyes, who was at pains to stress he was happy with the squad he inherited from Alex Ferguson.

"That's the squad that finished 15 points clear at the top of the Premier League. I'm confident with that squad, from what I've seen. They've got a great squad of players," he said.

United cancelled an open training session at the 40,000 -seat Hong Kong Stadium that had been scheduled for Sunday because of the poor state of the pitch, where Spurs defender Jan Vertonghen was hurt on Wednesday.

Moyes played down fears one of his players might also fall victim to the surface, following several days of heavy rain in Hong Kong.

"We are used to playing on good surfaces and good pitches, but it was the weather that didn't help. There was nothing the people here in Hong Kong could do to make it any better," he told a packed press conference.

"The weather was terrible for three or four days as far as I know. It's drying out now, which might in a way make it worse if it became bobbly.

"But we will play. The players have been brought up on all sorts of pitches, though I do take the point that these days the quality of the surfaces tend to be very good."

He expects to pick a strong side for Monday's game, which comes after matches in Thailand, Australia and Japan.

United have lost twice, drawn once and won only once so far on tour, but England defender Phil Jones was unconcerned and said Moyes had been stamping his mark on the squad.

"We have been together four or five weeks now and we've had some really good training sessions and he's implemented what he wants to do in training and games," said Jones.

"You can see things coming off in games and come the start of the season I'm sure we'll be ready to go and firing again."

SOURCE:AFP

"WALIOPENDEKEZA SERIKALI TATU NI WAZEE WANAOSUBIRI KUFA"...NAPE NNAUYE

 
MZIMU wa serikali tatu bado unaendelea kukitesa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo jana, Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alipinga tena uwepo wa serikali tatu na kudai kuwa waliotoa maoni hayo ni wazee wanaosubiri kufa. 


Akizungumza jijini Dar es Salaam katika kongamano la Umoja wa Vijana (UVCCM) la kujadili mchakato wa Katiba Mpya, katika ukumbi wa Arnatouglo, Nnauye alisema nia ya serikali tatu ni kuleta matabaka ambayo yatasababisha migogoro.

“Wazee hawa wanaosubiri kufa wanataka kutuletea matabaka, vijana ndio nguvu kazi ya taifa, kitendo cha kuwepo kwa serikali tatu ni kusababisha mgogoro, kwa nini wasingevunja Muungano enzi za ujana wao? Wamenufaika na Muungano kwa kipindi cha miaka 50, sisi vijana wanataka kutuachia mgogoro!”alisema Nnauye.

Nape alisema kuvunjwa kwa Muungano kutasababisha mgogoro mkubwa wa rasimu kutokana na muda ambao Muungano huo umedumu.

Alisema kuundwa kwa serikali tatu si sera ya CCM kama wanavyodai wapinzani, bali ni maoni ya watu waliyoyawasilisha katika ukusanywaji wa maoni ya Rasimu ya Katiba mpya.

“Sera ya CCM ni kuongoza serikali mbili na si tatu, na hii sera tutaendelea kuitetea na kuilinda mpaka mwisho wa dunia, tunachoamini katika chama chetu hatuogopi kutetea sera ambazo tumezitoa wenyewe,” alisema Nnauye.

Alisema ni vyema zikamalizwa kasoro zilipo katika mfumo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na si kuongeza madaraka yasiyo na tija.

Nape alisema kitendo cha Tume ya Jaji Joseph Warioba kusema imetumia sheria ya mwaka 1964 kuwa kigezo cha kuundwa kwa serikali tatu si sahihi, kutokana na makubaliano ya mwaka huo kwamba ni serikali mbili.

Kiongozi huyo wa CCM pia alishangazwa na kitendo cha Rasimu ya Katiba mpya kutamka wazi idadi ya mikoa pamoja na wilaya ambazo zitatumika katika uchaguzi na kwamba mwenye jukumu hilo ni Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.

“Serikali ya Muungano chini ya mfumo wa serikali tatu itaelea katika madaraka, kwani serikali ya Tanganyika itakuwa haiwezi kuwatetea wananchi, hali itakayosababisha kuwepo kwa mgogoro mkubwa wa urasimu ambao ni adui wa maendeleo,” alisema Nnauye.

Aidha alisema kuwa kuvunjika kwa Muungano kutasababisha kuiburuza Serikali ya Zanzibar kiuchumi, kwani asilimia 95 ya uchumi wa visiwani unategemea Tanzania Bara.

Alisema kuwa sera nzuri ya kuwa kiongozi ni kuwatetea wananchi na si kuwazidishia mizigo.

Akizungumzia suala la mgombea binafsi, Nnauye alisema CCM hakiogopi mgombea binafsi, kwani hata akigombea chama hakitapata hasara yoyote.

Nape alisema sera ya CCM ni kukataa wagombea binafsi wanaouza unga na si kukataa mgombea binafsi kama ambavyo vyama vingine vya siasa vinavyodai katika vyombo vya habari.

Alisema katika Rasimu hiyo sura ya 9 inazungumzia umri wa Mbunge kuwa kuanzia miaka 25, lakini kwa CCM suala hilo si sahihi, kwani wabunge wenye miaka 21 wanawajibika vizuri kuliko wazee.


Mtanzania

WATHUMIWA WALIOKAMTWA NA MADAWA YA KULEVYA CHINA NA HONG KONG WAFUNGUKA NA KUANZA KUWATAJA WAKUBWA WAO

    
                        Mbunge wa Kinondoni-CCM, Iddi Azan
Mbunge Wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania kutoka jimbo la Kinondoni, inasemekana ametajwa na wafungwa wa kitanzania waliofungwa jela huko nchini Hong Kong kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya.

Taarifa hiyo iliyomhusisha Mbunge huyo na mtandao huo mkubwa wa biashara hiyo ya madawa ya kulevya nchini Tanzania, ilitolewa katika barua maalum iliyoandikwa na mmoja wa Wafungwa katika magereza ya nchini Hong Kong ambapo inasemekana kuna wafungwa wa kitanzania wanaofikia 200.

Kati ya hao wafungwa 200 waliopo magerezani na vizuizini, 130 tayari wameshahukumiwa na 70 bado wanasubiri kesi zao kutajwa. Kuanzia Mwezi wa Tano mpaka wa Sita mwaka huu wa 2013, tayari Watanzania wapatao 50 wameshakamatwa na madawa ya kulevya wakati wakijaribu kuingia katika viwanja vya ndege vya nchi za China na Hong Kong.

Mbali na Hong Kong, pia kumekuwepo na taarifa mbalimbali za raia wa Tanzania ambao wamekatwa na madawa ya kulevya nchini Afrika ya Kusini na kwingineko duniani. Mmoja kati ya waliokamatwa na madawa hayo ni mwanadada mahiri wa Kitanzania ambaye alikuwa mrembo katika video mbalimbali za Bongo Flava anayeitwa Agnes Gerald au kama anavyojulikana na wengi kwa jina la Masogange.

Waraka huo wa mfungwa huyo wa Kitanzania pia umeorodhesha idadi kubwa ya wafanyabiashara wengine nchini Tanzania ambao ni wahusika wakubwa katika biashara hii haramu ya madawa ya kulevya.

Madawa hayo ya kulevya yanasemekana yanaingizwa nchini Tanzania kwa wingi kwa njia ya meli na boti mbalimbali yakitokea katika nchi za Pakistan, Afghanistan na nchi nyingine za Mashariki ya mbali.

Ni muhimu kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzisha kampeni kubwa ya kuwakamata wahusika wote katika biashara hii na kuwafikisha katika vyombo vya sheria, athari za madawa hayo zimezidi kuonekana sehemu mbalimbali nchini Tanzania na dunia nzima.

Soma barua iliyowataja wafanyabiasha hao wakubwa wa madawa ya kulevya nchini Tanzania hapo chini.




SOURCE:Bongo celebrity

Saturday 27 July 2013

Mkiambiaji Kenya azirahi uwanjani

 

Mwanariadha wa Kenya wa mbio za masafa marefu Irine Chebet Cheptai amekimbizwa hospitalini baada ya kuzirai katika mbio za uwanja wa Olimpiki.

Cheptai ambaye alikuwa kuwa mmoja wa wanariadha walioshiriki katika mbio za mita elfu tatu alizirai muda mfupi baada ya kumaliza mbio hizo ambapo alimaliza katika nafasi ya kumi na moja na kuweka muda wake kasi zaidi katika mbio hizo wa dakika nane na sekunde ishirini.
Madaktari waliokuwa uwanjani walimtibu mwanariadha huyo aliyekuwa amepoteza fahamu kabla ya kumkimbiza hospitalini kwa machela.
Ripoti zinasema Cheptai hatimaye alipata fahamu akipokea matibabu hospitalini.
Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka ishirini na moja hushiriki katika mbio za mita elfu tano na mwaka huu tayari ameshiriki katika mashindano mawili ya dunia ya IAAF Diamond League.
Mwezi Mei mwaka huu mjini Shanghai, Cheptai aliandikisha muda wa dakika kumi na nne sekunde hamsini nukta tisa tisa, muda ambao ndio bora zaidi aliouandikisha katika mbio hizo.
SOURCE:BBC

AirAsia Japan cancels hundreds of flights


AirAsia Japan has said the budget carrier will cancel hundreds of flights over two months before it ceases operations under the current brand at the end of October.
AirAsia Japan, operated jointly by Malaysia-based AirAsia and major Japanese carrier All Nippon Airways (ANA), will suspend 14 daily flights from September 1 to October 26, according to a company statement.
The carrier said the cancellations, which will reportedly affect 14,000 passengers, was because of a lack of planes to service all its routes.
The affected routes include flights linking Seoul to the central Japanese city of Nagoya and Tokyo to the northern city of Sapporo.
The carrier will cease operations by the end of October, just over a year after it started flying out of Tokyo's Narita airport in August.
Announcing the dissolution of AirAsia Japan in June, the Malaysian carrier cited a "fundamental difference of opinion between its shareholders on how the business should be managed, from cost management to where the domestic business operations should be based".
ANA however said the venture dissolved because it was not well known in Japan and could not register profits.
The Japanese carrier plans to launch a new budget brand in November.
SOURCE:AFP

DJ Khaled, asked Nicki Minaj to marry him via a video posted online and he explained why he wants Nicki as his wife...

 
Publicity stunt or is he for real? 37 year old record producer, rapper, DJ and record label executive, Khaled bin Abdul Khaled, better known by his stage name DJ Khaled, asked Nicki Minaj to marry him via a video posted online and he explained why he wants Nicki as his wife...

"I want to be honest with you. I love you. I like you. I want you to be mine. The only reason I'm not telling you this face to face is because I know that you're busy. You need a man like me in your life that’s gonna take care of you and respect you. You gotta take your time and think about it, I understand... but I know I have to be here today to let you know how serious I am and about how serious this is to me. I want to let your fans know, my fans know, my family, your family, that I wanna marry you. I been working hard to get this ring... Nicki Minaj... will you marry me?'
DJ Khaled popped the question with a $500,000 diamond ring and with help from MTV. Nicki hasn't responded yet. The two recently worked together on Nicki's latest single 'Twerk It'. See his proposal video after the cut...he sounds damn serious

MTANZANIA MWINGINE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA HONG KONG

 Mtu mmoja jana alisema sasa hivi wasafiri watokao Tanzania wanakaguliwa kwa makini zaidi ya ilivyokuwa hapo awali kutokana na matukio ya kukamatwa na dawa za kulevya! Hii ni sifa mbaya mno kwa raia na Taifa zima!

Iliyopachikwa hapo chini ni taarifa kutoka kwenye tovuti ya Serikali ya Hong Kong ya Julai 26, 2013

Hong Kong Customs yesterday (July 25) detected three drug trafficking cases, with seizures totally valued at $4.78 million, in the department's escalated anti-narcotics efforts to combat drugs.

     Customs officers at the Hong Kong International Airport (HKIA) intercepted a 26-year-old incoming male passenger arriving from Tanzania for clearance yesterday afternoon and seized 1.6 kilogrammes of heroin concealed in two false compartments of his hand carry briefcase.
The drugs would fetch a value of about $1.28 million.

     Later in the evening, Customs officers at the HKIA intercepted another 45-year-old man from Tanzania for clearance. On suspicion of concealment of drugs inside his body, the suspect was escorted to hospital where he discharged 204 grammes of heroin after staying for one day. The value of the drugs was about $0.16 million. The suspect is still in the hospital.

     In the same evening, Customs officers intercepted a 28-year-old man at a carpark in Tai Kok Tsui. Approximately 2.03 kg of cocaine camouflaged as snacks were found inside a plastic bag carried by him.

     Customs officers later escorted the suspect to a domestic flat nearby for a search and seized 1 kg of cocaine and 290 grammes of crack cocaine there. The total value of the seizure was about $3.34 million.

     A Customs spokesperson said today (July 26) that all three suspects in the three cases were arrested for drug trafficking. The cases are still under investigation.

     Under the Dangerous Drugs Ordinance, drug trafficking is a serious offence. The maximum penalty is life imprisonment and a fine of $5 million.


Ends/Friday, July 26, 2013
Issued at HKT 23:43


--Via wavuti.com

PROGRAM YA AJIRA KWA VIJANA WALIOHITIMU VYUO VIKUU NCHINi

PROGRAMU YA AJIRA
Programu hii itatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na vyuo vya elimu ya juu nchini,Taasisi za fedha na wabia wa maendeleo.Kwa kuanzia utekelezaji wake utaanza kwa kuendeleza programu ya mfano iliyoanzishwa na Idara ya kilimo, uchumi na Biashara katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (DAEA-SUA) na hatimaye kuwafikia wahitimu wa vyuo vingine vya elimu ya juu katika kipindi husika.

Kwa kuanzia serikali imekubaliana na Benki ya CRDB kuanza utoaji wa mikopo kwa vijana mara  utekelezaji wa programu utakapoanza.

Kwa kuwa kasi ya wanaojiunga elimu ya juu nchini imeongezeka wastani wa (48% kwa mwaka) na Wizara imeona vijana wanapomaliza elimu ya juu wanakuwa na elimu ya nadharia katika fani walizozisomea, tumeona kuna umuhimu wa elimu ya ujasiriamli, mitaji na maeneo ya kufanyia uzalishaji na biashara ambavyo ni msingi wa programu hii. Programu hii ni bora kwa kuwa ina vigezo vya ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji.

MADHUMUNI YA PROGRAMU.
Ni mojawapo ya hatua za utekelezaji wa sera ya Taifa ya Ajira ya mwaka 2008 ya kuhamasisha uzalishaji wa

kitaifa kufanikisha Ajira kamili yenye kipato na iliyochaguliwa kwa uhuru,kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira na ajira isiyokidhi viwango na kuongeza tija sehemu za kazi.

LENGO:
Lengo kuu la program ni kuongeza fursa za Ajira 30,000 za moja kwa moja kwa vijana wahitimu wa elimu ya juu kwa kipindi cha miaka mitatu (3) na kuwawezesha vijana kujiajiri na hata kuajiri vijana wengine kutokana na miradi watakayoibuni wao wenyewe.
                                                                  
Malengo mengine ni:-
1.Kuongeza idadi ya vijana wanaomiliki shughuli rasmi za kiuchumi na wamejiajiri na kuajiri wengine.
2. Kukuza utamaduni wa kijasiriamali pamoja na ubunifu.
3.Kuhamasisha matumizi bora ya nguvu kazi.

PROGRAMU INALENGA.
Programu hii inalenga vijana wa elimu ya juu ambao wapo tayari kuanzisha shughuli za kujiajiri katika sekta ya kilimo cha mazao, ufugaji, uvuvi, misitu na usindikaji.

MIRADI.
Miradi itakayoanzishwa itatoa ‘Mnyororo mzima wa thamani’ au INTERGRATED CROSS VALUE CHAIN (ICVC)
Kwa mfano,mradi wa Alizeti na ukamuaji mafuta.
1st step- Uandaaji mashamba,ulimaji,upandaji,palizi na uvunaji
2nd step- Usafirishaji, uhifadhi, usindikaji
3rd step- Ukamuaji mafuta, ufungashaji na uuzaji mafuta.

MAHITAJI YA RASILIMALI.
Jumla ya shilingi bilioni 54.451 zitahitajika kwa kipindi cha miaka 3 ya utekelezaji wa programu ambapo shilingi Bilioni 50 zitawekwa dhamana na shilingi bilioni 4.451 zitatumika katika mafunzo na kuwaandaa vijana ili waweze kukopesheka

MATOKEO YA PROGRAMU HII.
      I. Vijana watajengewa uwezo wa kujiajiri katika sekta zilizotajwa za kilimo, usindikaji, uvuvi na maeneo mengine kama vile viwanda vidogo na vya kati.
     II. Kuongezeka kwa fursa za Ajira nchini na kupungua kwa kiwango cha umaskini.
    III. Kupungua kwa matukio ya uhalifu na vitendo visivyokubalika katika jamii.
    IV. Kupungua kwa kasi ya vijana kuhamia mjini na kuimarika kwa uchumi wa nchi.


MATOKEO TARAJIWA YA PROGRAMU.
Programu hii ya wahitimu wa elimu ya juu itatoa fursa za Ajira kwa wahitimu 30,000 kutokana na miradi 1,000 kwa kipindi cha miaka 3.
Uzoefu unaonesha kuwa mradi mmoja wa kilimo wenye thamani ya sh. milioni 50 una uwezo wa kutoa ajira kwa wahitimu 20 hadi 30.

PROGRAMU ITATEKELEZA KATIKA AWAMU 3.
(a) Awamu ya kwanza itahusisha vijana wahitimu 600 kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA)    kumiliki miradi 200 ya kujiajiri na kuajiri wahitimu wengine wasiopungua 5,400 kutoka maeneo mengine.
 (b)  Awamu ya pili imelenga kuwawezesha vijana 900 wa elimu ya juu kutoka vyuo vingine ambao watakua tayari kuanzisha miradi ya kujiajiri na kuajiri wengine .Ambapo Miradi 300 itawezesha kuzalisha ajira za moja kwa moja kwa vijana wahitimu wasiopungua 8,100.Hapa miradi itahusisha sekta nyingine zitakazoonekana zina tija na kuongeza fursa za ajira.
(c) Awamu ya tatu imelenga kuwawezesha vijana wahitimu 1,500 wa vyuo mbalimbali vya kati vikiwepo vya VETA. Jumla ya miradi 500 itawezeshwa na kuzalisha ajira kwa vijana 13,500.

PROGRAMU ITAJUMUISHA YAFUATAYO.
    I. Utambuzi na uhamasishaji vijana—ambapowataandikishwa kupitia mikoa na Wilaya wanayoishi
   II. Kutoa mafunzo ya ujasiria mali na stadi zakazi-mafunzo yatatolewana SUA,baadae kwani kubuni na kuandaa andiko la Biashara (Business proposal)
   III. Kujenga uwezo wa vijana kulingana na miradi waliyoainisha –lengo ni kuwapatia ujuzi na uzoefuwa namna ya utekelezaji miradi.
   IV. Mafunzo na uzoefu kwa waendeshaji wa program-Wahusika watajengewa uwezo kujifunza kutokana na miradi ya ukuzaji ajira katika nchi nyingine.Taasisi husika Wizara ya Kazi na Ajira,Benki ya CRDB,SUA na SUGECO.
    V. Kutoa mafunzona huduma za kitaalamu na uratibu katika maeneo ya uzalishaji.

UTARATIBU WA UKOPESHAJI.
- Program hii ni ya miaka 3 na mikopo itakayotolewa ni ya miaka 3 na urejeshwaji wa mikopo ni kuanzia miaka3 hadi 5.
-Muda wa mkopaji kurejesha mkopo ni kuanzia miezi 6 hadi mwaka 1 kutegemeana na aina ya mradi.
-Utaratibu wa ukopeshaji ni wastani wa sh. mil 50 hadi 300mil kulingana na mradi.
Utaratibu wa utekelezaji na viwango vya riba utaainishwa katika mpango kazi wa utekelezaji programu.

Friday 26 July 2013

Mmiliki wa home shopping center aliyemwagiwa tindikali apelekwa afrika kusini kwa matibabu zaidi...!

Mfanyabiashara maarufu na Mmiliki wa maduka ya Home Shopping Center(HSC), Said Mohamed Saad, ambaye wiki iliyopita alimwagiwa tindikali maeneo ya Msasani City Mall, jijini Dar es Salaam, sasa yuko Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

Hali yake inadaiwa kuendelea vizuri, lakini kuna uwezekano wa jicho lake moja kutokuona kabisa baada ya kuathirika sana, lakini jicho la pili liko salama.



Wiki iliyopita majira ya saa moja jioni, mfanyabiashara huyo alimwagiwa tindikali na mtu mmoja ambaye hakufahamika na mara baada ya kutenda tukio hilo, mhusika alikimbia huku mlinzi wa eneo hilo akijaribu kumkimbiza pasipo mafanikio baada ya kuteleza na kuanguka.

Hatua hiyo ilitoa mwanya kwa mtuhumiwa kutoroka eneo la tukio kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki.

Hapo awali ilidaiwa kuwa Saad alikuwa anaweza kuzungumza japo amefungwa mashine sehemu ya pua kwa ajili ya kumsaidia kupumua.

Matukio ya watu kumwagiwa tindikali yameonekana kushamiri nchini katika siku za hivi karibuni.

Tukio la kumwagiwa tindikali mmiliki huyo wa Home Shopping Centre, limekuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Said Juma Makamba naye ajeruhiwe vibaya usoni kwa kumwagiwa maji maji yanayosadikiwa kuwa ni tindikali majira ya usiku akiwa nyumbani kwake

SOURCE:Gumzo la Jiji

Maandamano yafanyika nchini Tunisia

 

           Mohamed Brahmi

Tunisia inashuhudia mgomo wa taifa zima baada ya kuuawa kwa kiongozi wa upinzani Mohamed Brahmi.

Chama cha wafanyakazi kikubwa kuliko vyote nchini Tunisia, UGTT, kimetoa wito wa kuwataka wananchi kupinga "ugaidi, ghasia na mauaji".

Alhamisi polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji katika miji kadhaa nchini humo, baada ya Bwana Brahmi kuuawa kwa kupigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Tunis.

Chama tawala nchini Tunisia, cha Kiislam cha Ennahda kimekanusha tuhuma kutoka kwa ndugu wa marehemu kuwa kilikula njama katika mauaji ya Bwana Brahmi.

SOURCE:BBC

Jeshi la Misri latoa onyo kali kwa raia

 Jeshi la Misri limeonya kuwa litatumia nguvu dhidi ya makundi yatakayosababisha ghasia na machafuko wakati wa maandamano ya leo.

Mkuu wa majeshi Jenerali Abdel Fattah al-Sisi ametoa wito kwa raia wa nchi hiyo kuandamana katika b arabara za mji kuunga mkono juhudi zao za kukabiliana na vitendo vya kigaidi.

Wafuasi wa rais aliyeondolewa madarakani, Mohamed Morsi vile vile wanatarajiwa kushiriki katika maandamano hayo.

Bwana Morsi amekuwa akizuiliwa na jeshi tangu tarehe tatu mwezi huu.

Mwendesha mashtaka mkuu wa serikali amesema, Bwana Morsi anazuiliwa kuhusiana na uhusiano na wapiganaji wa Kiislamu wa Hamas nchini Palestina.

Shirika la habari la serikali, Mena, limesema Bwana Morsi anachunguzwa kufuatia madai kuwa anashirikiana na kundi hilo la Hamas kushambulia vituo kadhaa vya polisi na magereza wakati wa mageuzi ya mwaka wa 2011.

Lakini chama chake cha Muslim Brotherhood, kimesema kuwa kilipata msaada kutoka kwa raia wa nchi hiyo kushambulia magereza na wala sio raia wa kigeni kama inavyodaiwa.

Maandamano nchini Misri

Kiongozi huyo kwa kwanza kuwahi kuchaguliwa kwa njia ya Kidemokrasia kuongoza Misri, aliondolewa madarakani baada ya raia wa nchi hiyo kuandamana wakati wa sherehe za kuadhimisha mwaka mmoja tangu alipochukua madaraka.

Tangu wakati huo, Bwana Morsi amekuwa akizuiliwa na jeshi la nchi hiyo katika eneo lisilojulikana.

Shirika hilo la Mena limesema agizo lilitolewa kwa rais huyo kuzuiliwa kwa muda wa siku kumi na tano.

Mwandishi wa BBC mjini Cairo anasema kuwa tangazo hilo sasa limeondoa wasi wasi kuhusiana na hatma yake, hasa kufuatia shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa ya kutaka rais huyo wa zamani kauchiliwa huru an kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa sheria za nchi hiyo.

Msemaji wa jeshi Kanali Ahmed Mohammed Ali amesema jeshi la nchi hiyo litaruhusu maandamano ya amani lakini ameonya kuwa watakabiliana vikali na kundi lolote ambalo litajaribu kusababisha machafuko.

SOURCE: BBC

Polisi wamnasa muuaji wa kukodiwa

JESHI la Polisi mkoani Katavi limemtia nguvuni Masaga Charles (36) akidaiwa kuwa muuaji wa kukodiwa. Charles ambaye pia alikuwa bingwa wa mashindano ya mbio za baiskeli yaliyofanyika Arusha mwaka jana, anatuhumiwa kufanya mauaji ya ukatili wilayani Mpanda.

Inaelezwa kuwa kwa zaidi ya miaka 15, Charles amekuwa akishiriki katika mashindano ya mbio za baiskeli katika mikoa ya Tabora, Shinyanga, Mwanza na Arusha Oktoba mwaka jana ambako aliibuka mshindi na kujinyakulia Sh 800,000.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi , Dhahiri Kidavashari, mtuhumiwa huyo ni mkazi wa Kijiji cha Chilalo Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Charles anatuhumiwa kumuua Moshi Bella (44) wa Kijiji cha Karema kwa kumkatakata na panga kichwani na shingoni baada ya kuahidiwa kulipwa Sh milioni tano.

Kamanda Kidavashari alisema tukio hilo la mauaji ya kinyama lilitokea Julai 21 mwaka huu katika Kijiji cha Kabange Kata ya Simbwesa Tarafa ya Kabungu mkoani Katavi.

Alisema mtuhumiwa kabla ya kufanya mauaji hayo alionana na Bella akijifanya alikuwa anataka auziwe shamba.

Mazungumzo hayo yalifanyika Julai 20 mwaka huu nyumbani kwa Salumu Kajimba ambaye ni ndugu wa marehemu Bella, alisema Kamanda Kidavashari.

Kamanda alisema mtuhumiwa na Bella walikubaliana kuuziana ekari mbili za shamba ambalo ni mbuga ya mpunga.

“Walikubaliana kuuziana Sh 300,000 kwa kila ekari na baada ya makubaliano hayo mtuhumiwa alimuahidi Bella kwamba angerejea siku ya pili kwa ajili ya kutoa malipo hayo,” alisema Kamanda.

Alisema siku iliyofuata mtuhumiwa Charles alifika nyumbani kwa Salumu Kajimba ambaye ni ndugu wa Bella ya saa 9.00 alasiri lakini bahati mbaya Bella alikuwa amekwenda kisimani kuoga.

Mtuhumiwa baada ya kuambiwa Bella alikuwa amekwenda kisimani alimuaga Kajimba na mkewe akisema alikuwa anamfuata Bella.

Kamanda Kidavashari alisema Bella hakuonekana nyumbani tangu alivyowaaga kuwa anakwenda kuoga kisimani wala Bella aliyemfuata naye hakurejea hadi hapo mwili wa Bella ulipookotwa mbugani.

Mwili wa Bella ulikutwa umekatwakatwa na panga shingoni kwa nyuma na kichwani.

Kamanda alisema baada ya polisi kuarifiwa na raia wema kuhusu mauaji hayo waliweza kumkamata mtuhumiwa Masaga Charles katika mtaa wa Makanyagio mjini Mpanda.

Baada ya kukamatwa mtuhumiwa alikiri kuhusika na mauaji hayo akidai alitumwa na mkazi mmoja wa Kijiji cha Iroba Tarafa ya Kabungu wilayani Mpanda aliyemuahidi kumlipa Sh milioni tano.

Kamanda alisema mtuhumiwa alidai kuwa mtu aliyemtuma amekwisha kukimbilia mkoani Shinyanga ili asijulikane kuwa ndiye aliyehusika na mpango wa mauaji hayo.

Mtuhumiwa alidai kuwa kwa mara ya kwanza aliambiwa kufanya mauaji hayo Oktoba mwaka jana kwa malipo ya Sh milioni mbili lakini alikataa, alisema. Kamanda alisema mtuhimiwa alidai kuwa Aprili mwaka huu aliambiwa tena afanye mauaji kwa malipo hayo lakini akaendelea kukataa hadi alipoongezewa dau na kufika Sh milioni tano na kupewa shamba la ekari mbili.

Mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kujibu tuhuma za mauaji zinazomkabili, alisema kamanda.
source: Gazeti la mtanzania

Thursday 25 July 2013

Fabregas bid 'ongoing' - Moyes

 

Manchester United boss David Moyes said Thursday the English champions' attempts to sign Barcelona midfielder Cesc Fabregas remained alive after reports said two earlier bids had failed.

Moyes, who was appointed as Alex Ferguson's successor at the end of last season, tabled an initial offer of 25 million pounds ($38 million, 29 million euros), later upping the ante to 30 million pounds, British reports said.

Asked about any progress in United's talks with Barcelona on Spanish international midfielder Fabregas, Moyes simply said: "Ongoing".

Moyes is keen to sign the creative midfielder but reports from Spain suggest Barca will not make a decision on Fabregas until they appoint a successor to cancer-stricken coach Tito Vilanova,

Moyes also said Robin van Persie, who pulled out of United's last match on their Asian tour with a thigh-injury, was expected to play against Cerezo Osaka on Friday despite being absent from training.

Injured striker Wayne Rooney is on the mend, he added.

"Wayne is running, probably at the level where we thought he would be just now and he'll pick up his work again," he said.

Disaffected Rooney's withdrawal from the Red Devils' pre-season Asian tour with a minor hamstring injury has heightened speculation that a move away from Manchester United is imminent.

Rooney has been linked to rival club Chelsea, but United have made it clear they are not interested in selling him -- going so far as to post an eye-catching billboard on their Twitter account that announced his return for a friendly against Swedish side AIK Fotball on August 6.

United's second friendly in Japan comes on the heels of their 3-2 loss to Yokohama Marinos on Tuesday.

It was the Red Devils' second loss in three matches so far in their Asian tour which will wind up with a game in Hong Kong next Monday.

United's Japanese star Shinji Kagawa meanwhile looked forward to a return to the club where he began his career.

"Tomorrow, I will play against the side which helped me grow up and sent me to the world," the 24-year-old said. "I will give all I have as I know their supporters and coach are excited about it."

"I want to work hard and produce results in an effort to impress," said Kagawa, who had a disappointing first season with United scoring just six goals in 20 league matches.

source:AFP

Mbakaji sugu Afrika Kusini afariki

Mwanamume anayetuhumiwa kuwa mbakaji sugu nchini Afrika Kusini ,Sifiso Makhubo, amepatikana akiwa amefariki katika chumba chake gerezani.

Sifiso Makhubo, aliyekuwa anakabiliwa na mashtaka 122 ikiwemo mauaji na ubakaji alipatikana akiwa amejinyonga kwa blanketi.

Baadhi ya makosa aliyoshtakiwa nayo ni pamoja na kuwaambukiza waathiriwa virusi vya HIV

Afrika Kusini ina moja ya visa vingi zaidi vya ubakaji duniani, huku polisi wakionyesha kuwa ni visa 64,000 pekee ambavyo viliripotiwa mwaka jana.

Maafisa wanasema kuwa alikuwa peke yake katika seli yake , lakini wanachunguza kilichosababisha kifo chake.

Bwana Makhubo anatuhumiwa kwa kuwabaka watoto 35 na wanawake wawili, kati ya Januari mwaka 2006 na Februari 2011.

Hadi sasa uchunguzi uliofanywa wa DNA katika waathiriwa waliodai kubakwa naye, ulithibitisha kuwa yeye ndiye alikuwa mbakaji.

BBC

Sitta ahoji harambee za Lowassa Makanisani na sasa misiktini

 

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amehoji walipo na majina ya wanaoitwa “Marafiki wa Lowassa” wanaomchangia mamilioni ya fedha za kusaidia harambee mbalimbali nchini.

Akizungumza na Raia Mwema wiki hii, Sitta alisema ni ajabu kwamba ‘marafiki’ hao wamekuwa wakitajwa tu bila ya kufahamika ni akina nani, wana ukwasi kiasi gani na wameupataje ukwasi huo.

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, amekuwa akichanga michango ya fedha katika harambee mbalimbali nchini huku akisema fedha anazochanga si zake binafsi bali ni michango pia ya rafiki zake.

Na akizungumza kupitia kwa msaidizi wake jana Jumanne, Lowassa alisema hoja kwamba marafiki zake wanaomchangia hawafahamiki haina ukweli wowote kwa kuwa amekuwa akiwataja hadharani kwa majina kila wanapomchangia.

Lakini Waziri Sitta alihoji, alisema ya kuwa, haiingii akilini watu kumchangia mwanasiasa huyo bila ya kuwa na sababu za msingi za kufanya hivyo.

“Nyie waandishi mnatakiwa mlisaidie taifa kwenye hili. Mtu anapita nchi nzima anachanga mamilioni ya fedha na anasema si zake bali ni za rafiki zake. Lakini hatuambii rafiki zake hao ni akina nani. Hatujui kama hata rafiki zake hao wanachangia kodi kwa serikali.

“Lakini, swali kubwa la kujiuliza zaidi hapa ni hili; inakuaje michango ya kwenye taasisi za kidini mtu ampe Lowassa na asiende mwenyewe kutoa kanisani au msikitini kwake?

“Ninachojua mimi, mbinguni hakuna c/o (kupitia kwa). Ina maana Wasamaria hawa wanajua kwamba ili uende mbinguni ni lazima mchango wako utolewe na huyo bwana (Lowassa)?” alihoji Sitta.

Katika mahojiano hayo, Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa wakati wa kashfa ya Richmond iliyomwandama Lowassa, alisema kizazi cha Watanzania wa sasa kina shida kubwa kwenye kupata viongozi walio waadilifu.

Alisema uongozi sasa umekuwa fursa ya kuchuma mali badala ya kutumikia umma, na kwamba hata katika matukio ya kuongeza heshima kwa taifa, watu wanayatumia kutia aibu taifa.

Sitta aliyasema hayo akigusia vitendo vya ufisadi vilivyofanyika wakati wa mkutano wa Smart Partnership uliofanyika nchini mapema mwezi huu ambapo ripoti za vitendo vya ufisadi zimeanza kuibuka.

“Mkutano ule ulitakiwa ujenge heshima yetu. Lakini majizi yameingia na sasa taifa limeingia katika kashfa nzito. Kila kitu sasa ni ufisadi tu. Tukiendelea hivi hivi hatutafika kokote,” alisema mwanasiasa huyo.

Kauli hiyo ya Sitta imekuja huku Lowassa akizidi kuchanja mbuga katika kuendesha harambee ndani ya makanisa na misikiti, na mara kwa mara harambee anazoendesha na kufanikisha ni zaidi ya shilingi milioni 200.

Kwa mfano, hivi karibuni akiwa jijini Mwanza Lowassa alifanya harambee ya Sh. milioni 590, ikiwamo michango yake na watu anaowaita “rafiki zake”, lakini pia amewahi kufanya harambee mkoani Ruvuma, wilayani Nyasa, ambako zilikusanyaswa Sh. milioni 300.

Lowassa pia amewahi kufanya harambee kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa Katoliki Nyakato Mwanza ambako alichangisha Sh. milioni 200, amewahi kuchangisha Sh. bilioni moja kwa ajili ya Chama cha Kuweka na Kukopa (Saccos) cha Walimu wa Moshi Vijijini. Amewahi pia kuendesha harambee na kukusanya Sh milioni 134 Babati, mkoani Manyara.

Ingawa Lowassa binafsi amewahi kunukuliwa akisema si tajiri wa fedha isipokuwa ni tajiri wa watu, anatajwa kumiliki biashara kadhaa kubwa pamoja na mali nyingi kama majumba katika maeneo mbalimbali nchini.

Alipotafutwa Lowassa, ili pamoja na mambo mengine, aweze kutoa ufafanuzi juu ya baadhi ya hoja hizo zilizoibuliwa na Sitta dhidi yake, mwanasiasa huyo alimwelekeza mwandishi wetu kuzungumza na Katibu wake, aliyejitambulisha kwa jina la Boniface Chami.

Akijibu ni kwa nini Lowassa hawataji hadharani marafiki zake hao wanaodai wanamchangia mamilioni ya shilingi anayoyatoa kwenye harambee zake, Chami, alisema hoja hiyo haina ukweli wowote kwa kuwa Lowassa amekuwa akiwataja hadharani kwa majina marafiki zake hao wanaomchangia.

Alitoa mifano ya harambee zilizoendeshwa na Lowassa kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa makanisa katika mikoa ya Morogoro na Shinyanga, na hii ya hivi karibuni aliyochangia ujenzi wa kituo cha Radio Ikra, kinachomilikiwa na Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA), na harambee yake kufanyika jijini Mwanza.

“Miongoni mwa marafiki zake waliomchangia katika harambee ya kuchangia kanisa mjini Morogoro ni Philemon Molel. Huyu alimwinua pale pale na kumshawishi achangie, na akachanga pesa nzuri,” alisema Chami na kuongeza:

“Kule Shinyanga, wakati wa harambee ya Kanisa la KKKT, alimtaja hadharani rafiki yake Mathias Manga. Huyu ni mfanyabiashara mkubwa wa madini jijini Arusha, lakini pia anamiliki hoteli moja kubwa ya kitalii jijini Mwanza, inayoitwa Gold Crescent, na hata kwenye harambee ya juzi jijini Mwanza kuchangia Kituo cha Radio Ikra, rafiki yake huyu huyu alimtaja pia hadharani, na mbali na kutoa ukumbi wa hoteli yake utumike kuendeshea harambee ile, alichangia pia shilingi milioni 10.

“Hiyo ni mifano michache tu, lakini wako wengi, na naamini hata nikiwataja wote hapa, kesho hawatakanusha kama ambavyo marafiki zake aliowataja (Sitta) kule kwenye harambee yake jijini Mwanza walivyokanusha. Kila Mtanzania anakumbuka, Sitta alimtaja Magufuli (John) kuwa ni rafiki yake na alikuwa amemchangia shilingi milioni tano, lakini kesho yake akakana.”

Kuhusu ni nini wanatarajia kupata kutoka kwa Lowassa marafiki zake hao wanaomchangia. Chami alijibu: “Hawatarajii kupata chochote kutoka kwa mheshimiwa zaidi ya mapenzi waliyonayo kwake. Siku zote amekuwa akisisiza kuwa hana utajiri ila utajiri wake ni watu, watu wanapenda kuchangia harambee zake kwa sababu ya ushawishi wake tu, basi.