Monday, 5 August 2013

JAJI FRANCIS MUTUNGI ATEULIWA KUWA MSAJILI MPYA WA VYAMA VYA SIASA...


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji Francis S.K. Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Taarifa iliyotolewa Dar Es Salaam leo, Jumatatu, Agosti 5, 2013, na kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.

Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria.

Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu, DAR ES SALAAM

Saturday, 3 August 2013

NCHEMBA ATUHUMIWA KUSHUSHA HESHIMA YA CCM

 

MATUKIO kadhaa ya kisiasa, mwelekeo, kauli na mienendo ya baadhi ya wanasiasa waandamizi na wenye nguvu katika Chama cha Mapinduzi (CCM) vimeibua mkanganyiko na hali tete ndani ya chama hicho, Tanzania Daima Jumamosi limebaini.

Kwa muda sasa, kumekuwa na minyukano ya ndani kwa ndani miongoni mwa viongozi waandamizi wa CCM, huku baadhi yao wakilaumiana kwa “kuchafua na kuua” chama.

Baadhi yao wamefikia hatua ya kumlaumu Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuwapa madaraka makubwa baadhi yao, na kushindwa kuwanyang’anya pale wanapoonyesha dalili za “kuua” chama chao.

Gazeto hili linazo taarifa za baadhi ya viongozi wastaafu wa CCM kupeleka ujumbe mzito kwa Makamu Mwenyekiti, Phillip Mangula, wakionyesha kukerwa na kauli au mwenendo wa baadhi ya viongozi waandamizi, hasa Naibu Katibu Mkuu, Mwigulu Nchemba.

Wanamtuhumu Nchemba kwa kushusha heshima ya CCM mbele ya umma, na kuchangia matokeo mabaya katika uchaguzi wa madiwani uliofanyika Arusha mwezi uliopita, ambako CCM ilishindwa na CHADEMA katika kata zote nne.

Baadhi ya wazee na makada waandamizi wanasema Nchemba ni “mzigo wa Kikwete,” kwa maana kuwa ndiye aliyempa madaraka, na ndiye anayemsikiliza na kumpa jeuri.

Nafasi anayopewa Nchemba imeleta mgongano wa chini kwa chini kati yake na Katibu wa itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ambaye kwa muda sasa amekuwa ndiye kipenzi cha Rais Kikwete katika kutekeleza mikakati kadhaa na kutoa matamko yenye utata dhidi ya viongozi au wanachama “wasiopendwa” ndani ya chama hicho, au dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kwa mujibu wa makada wanaokerwa na tabia ya Nchemba, kiongozi huyo amegeuka kero kwa viongozi wenzake, ambao wanasema ameingiza siasa za ujasusi wa waziwazi na mbinu nyingine chafu za kisiasa zinazomfanya aibomoe CCM na kuiongezea umaarufu CHADEMA mbele ya umma.

Source:Tanzania Daima

Rais mpya wa Iran ashika madaraka

 Hassan Rouhani

Rais mteule wa Iran Hassan Rouhani anaapishwa katika sherehe mjini Tehran ambapo atapewa idhini ya kiongozi wa kidini nchini humo, Ayatollah Ali Khamenei.

Rouhani ambaye alikuwa mpatanishi kwenye mazungumzo ya mradi wa nuklia wa Iran, alishinda uchaguzi wa urais nchini Iran katika duru ya kwanza.

Wakati wa kampeni zake rais huyo mteule aliahidi kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, na alisema ataimarisha uhusiano kati ya taifa hilo na jamii ya kimataifa ambao uliharibika zaidi wakati wa utawala wa Rais Mahmoud Ahmedinejad.

SOURCE:BBC

Bale bids Spurs teammates goodbye as Real deal looms

Tottenham take on Monaco on Saturday without Gareth Bale, who misses the pre-season friendly in the Principality through injury ahead of a likely defining week for his forecast world record transfer to Real Madrid.

The Wales superstar bid "an emotional farewell" to his teammates in London on Friday, autographing their shirts before they left for Monte Carlo, according to a report in The Sun.

The Spurs forward sits out Saturday evening's match, and may also miss Wales' friendly against Ireland in Cardiff on August 14, with a minor hamstring problem.

As Bale works on his fitness Tottenham chairman Daniel Levy will sit down for his first face-to-face talks with his Real Madrid counterpart Florentino Perez in Miami next week, possibly on Wednesday, The Times suggested.

Real are in Florida where Levy has a holiday home for a pre-season warm-up.

They are keen to see Bale at the Bernabeu ahead of their opening league game against Real Betis on August 18.

The 24-year-old is set to become the most expensive player of all time, an honour currently held by Cristiano Ronaldo who moved from Manchester United to Real for 94 million euros ($125 million, £82 million) in 2009.

Levy is reportedly holding out for a transfer fee in excess of £105 million while Real are looking to strike a deal at around £85 million with a makeweight, possibly Fabio Coentrao, thrown in.

On Friday, Arsenal manager Arsene Wenger claimed Bale's proposed mega transfer made a mockery of UEFA's Financial Fair Play rules.

It makes a joke of it. It's quite amazing that in the year where the Financial Fair Play comes in, the football world has gone completely crazy," the Frenchman said.

"You wonder what kind of impact and effect it has on the football world. It looks like it has made everybody worse than before."

SOURCE:AFP

World's second tallest building tops out in China


Work on the main structure of the world's second tallest skyscraper was completed on Saturday, as the final beam was placed on the Shanghai Tower.

A crane placed the steel beam 580 meters (1,900 feet) above the ground in Shanghai, China's commercial hub, as the building formally overtook Taiwan's 509 meter tall Taipei 101 building to become the highest tower in Asia.

Globally it is second only to the Burj Khalifa in Dubai, which stands at 830 meters. The tower, which costs an estimated $14.8 billion yuan ($2.4 billion), will reach over 630 meters when it is finally finished.

"It's a landmark and it will change the skyline of Shanghai," Xia Jun, of Gensler, the US firm which designed the tower, told a press conference on Saturday following a "topping out" ceremony.

"I don't think the importance of an architecture lies entirely in its height," he added.

The structure stands alongside China's previous tallest building, the 492 meter Shanghai World Financial Center -- and is due to open next year, by which time it may have been surpassed as the tallest building in China.


Chinese firm Broad Group have announced plans to construct an 838 meter tower in the central Chinese city of Changsha, which they say will be completed in April.

But reports in state-run media late last month said construction on the tower had been called off, because the building had not gained full local government approval.

The Broad Group called the reports inaccurate and said they had not been asked to halt construction in a statement sent to AFP this week.

Work on the Shanghai tower began in 2008, and its construction was partially backed by Shanghai's city government.

Concerns were raised last year when long cracks began to appear in the ground close to the building, prompting fears that ground around the tower was subsiding.

But Ding Jiemin, an architect who collaborated on the tower's design, played down fears on Saturday.

"These problems were just during construction period, it will not affect the security of the architecture," he said.

China is home to three of the world's 10 tallest buildings, according to research group Emporis -- which did not count the Shanghai Tower.

The Shanghai Tower's final beam was decorated with red ribbons and flags, and carried a banner which read: "Team of hoisting heroes".

SOURCE:  (AFP)

Friday, 2 August 2013

Kiwewe cha dhahabu Kewanja, Tanzania

Tanzania imekalia hazina. Nchi hiyo ya Afrika Mashariki ina akiba ya madini ya dhahabu wakia milioni 36. Katika orodha ya wazalishaji wakubwa wa dhahabu Tanzania inashika nafasi ya tatu nyuma ya Ghana na Afrika Kusini.

Lakini hadi sasa utajiri wa madini hayo haukuwanufaisha wananchi kutokana na kwamba migodi hiyo iko kwenye mikono ya makampuni ya kimataifa. Mwishoni mwa miaka ya 1990 serikali ya nchi hiyo imezivutia kampuni hizo za migodi kwa kupunguza kodi na leseni zake kuwa rahisi.

Hata hivyo kunakuwepo na mizozo kwenye sehemu nyingi za migodi kati ya kampuni hizo na wananchi wenyeji. Hususan hali hiyo imejitokeza kwenye mkoa wa Mara Kaskazini ulioko magharibi kabisa ya eneo la kaskazini magharibi mwa Tanzania kwenye mpaka na Kenya.Hapo kila kitu kinahusiana na dhahabu na kwamba kwa gramu chache tu za dhahabu watu wanakuwa tayari kuhatarisha maisha yao.

Wafanyakazi wavamizi

Wanasema wakati ni dhahabu ni masafa ya kama nusu saa kwa mwendo wa gari kutoka kijiji cha Kewanja hadi mpaka wa Kenya. Jumanne anauparamia mlima mkubwa wa kifusi cha migodi akiwa kama mita chache tu kufika juu. Kijana huyu ni mvamizi kwa sababu mlima wa vifusi aliokuwa ameuparamia unamilikiwa na kampuni ya dhahabu ya African Barrick Gold (ABG) tawi la kampuni kubwa kabisa ya kuzalisha dhahabu duniani ya Barrick Gold kutoka Canada. Mawe yalioko katika mlima huo ni taka kutoka kwenye mgodi ulio karibu ambapo hata hivyo huwa chini ya ulinzi wa kampuni hiyo.

Hazina chini ya ulinzi mkali: Mgodi wa dhahabu Mara Kaskazini

Hazina chini ya ulinzi mkali: Mgodi wa dhahabu Mara Kaskazini

Kwa wananchi wengi wanaoishi katika kijiji cha Kewanja katika mkoa wa Mara Kaskazini masalia hayo ni pato pekee kwao. Kila siku huuvamia mlima huo wa kifusi mara kwa mara kwa matarajio ya kupata mabaki kidogo ya dhahabu.

Kwa mujibu wa Jumanne mtu mmoja kati ya kila watu watatu ni mvamizi mahala hapo. Wengi kati yao ni vijana wa kiume na kuna na hata watoto. Jumanne ana umri wa takriban miaka 20 na huuza dhahabu anayoipata katika soko la kijiji ambapo hujipatia laki mbili za Tanzania kwa mwezi sawa na euro mia moja, kwa hiyo Jumanne ni miongoni mwa watu wanaojipatia kipato kikubwa katika mkoa huo.

Kuhatarisha maisha

Hata hivyo Jumanne anasema mzungu akimaanisha wamiliki wa mgodi huo amekuwa akiwabana sana wasichukue mawe yalioko kwenye mlima wa kifusi cha mgodi na kwamba watu wengine hupoteza maisha yao lakini maisha ni magumu na hawana njia nyengine ya kujipatia kipato.

Kuhatarisha maisha: Mwanamigodi katika kijiji cha Kewanja Kuhatarisha maisha: Mwanamigodi katika kijiji cha Kewanja

Eneo la kampuni hiyo ya dhahabu huwa liko chini ya ulinzi mkali ambapo hata polisi wa taifa hushiriki katika kutowa ulinzi huo. Walinzi hao huwa na mabomu ya kutowa machozi, risasi za mpira na na silaha nyengine kali. Kila mara watu huuwawa na wengine kujeruhiwa. Mwaka 2012 pekee kutokana na vyombo vya habari vya ndani ya nchi takriban watu wanane wameuwawa karibu na mgodi huo au kwenye mgodi wenyewe. Kwa wavamizi hasira inazidi kupanda ambapo mvamizi mmoja aliekataa kutaja jina lake amesema hakuna mtu anayejali juu ya watu walioko hapo na dio maana hupigwa risasi kama mbwa kwamba polisi hutekeleza kila wanachoagizwa na kampuni na wanakuwa kama vile ni vibaraka wao.

Donge nono

Kwa upande mwengine fedha nyingi hupatikana kutoka kwenye milima hiyo ya vifusi vya migodi. Mgodi huo wa Mara Kaskazini umekuwa na wamiliki mbali mbali hapo mwaka 2006 ulikuwa nchini ya mikono ya AGB. Kampuni hiyo zaidi ya muongo mmoja uliopita imekuwa ikijishughulisha nchini Tanzania na kwa hivi sasa pia inashughulikia migodi mengine minne ya dhahabu nchini humo.

Huko Mara Kaskazini kwa mujibu wa taarifa za kampuni hiyo wafanyakazi wa migodi 360 moja kwa moja wanatoka katika maeneo hayo na wengine zaidi ya 1,500 wakaazi wa hapo wanafanya kazi kwa njia ya mikataba na kampuni hiyo. Haata hivyo hiyo haiwezi kuitwa miujiza ya kazi. Mgodi huo hutowa ajira chache tu kwa wanakijiji 70,000 waliokuwepo kwenye vijiji vilio karibu na mgodi huo. Ingawa kampuni za migodi hupata fedha nyingi lakini hutowa ajira chache hili ni tatizo halisi katika sekta ya malighafi. Kwa mwaka 2001 pekee kampuni hiyo ya ABG imejipatia zaidi ya euro milioni 200 kutoka mgodi wake huo wa Mara Kaskazini.

2012_10_24_tansania_gold.psd

Miradi ya kijamii

Gary Chapman meneja wa mgodi anasema bila ya shaka kampuni hiyo inatakiwa kuwajibika kwa jamii na kwamba wanachukua hatua kujenga uaminifu baina yao na jamii ili kuheshimiwa na kuthaminiwa na jamii kwa nia ya kushirikiana na kuleta maendeleo. Kutimiza lengo hilo kampuni hiyo ina kitengo cha kushughulikia uhusiano na umma huko Mara Kaskazini ambacho kinaundwa na wafanyakazi 17 wa kiume na wa kike. Wafanyakazi hao wa masuala ya jamii hufanya ziara vijijini na kuwasiliana na wakuu wa vijiji na watu wenye kushughulikia jamii. Kitengo hicho kinasimamia miradi ya jamii ya kampuni hiyo. Kitu kimoja ambacho kampuni ya African Barrick Gold inajivunia sana ni shule ya sekondari ya Ingwe ambayo iko dakika chache kwa mwendo wa gari kutoka mgodi wao.

Anajivunia shule mpya: Mwalimu Mkuu Mageka 

 Anajivunia shule mpya: Mwalimu Mkuu Mageka

Kwa madarasa ambayo yamechakaa kampuni hiyo ya ABG imeyafanyia ukarabati hapo mwaka 2012 na hivi sasa wanashughulikia ujenzi wa ukumbi wa chakula na majengo zaidi ya shule kwa kutumia kampuni za kijenyeji kwa lengo la kuzalisha ajira zaidi. Hili ni jambo linalolitiliwa mkazo na kampuni hiyo ya AGB. Joash Mageka mkuu wa shule hiyo anafurahia mabadiliko mazuri kwana shule hiyo sasa inapendeza na kwamba pia idadi ya wanafunzi wanaokwenda kufanya kazi kama wavamizi imepunguwa. Anasema ingawa bado kuna wengine wanaoendelea kwenda wanajaribu kuwaelimisha juu ya umuhimu wa elimu na vipi inaweza kuwasaidia katika maisha yao ya baadae. Shule hiyo ni mradi wa kupigiwa mfano na kwa kampuni hiyo huo ni mfano wa maendeleo ya mkoa huo.

Mkoa unaendelea

Kwa mujibu wa taarifa za kampuni hiyo mwaka 2010 kampuni ya AGB imetowa dola milioni 20. 6 kwa ajili ya miradi ya jamii nchini kote Tanzania. Kiwango hiki ni chini ya aslimia moja ya faida inayopata kampuni hiyo. Idara ya uhusiano na umma ya kampuni hiyo inasema sehemu kubwa ya fedha hizo zimepelekwa Mara Kaskazini. Lakini hilo limetokea miaka miwili tu iliopita.Kwa nini halikufayika mapema zaidi hakuna mtu anayetaka kufafanuwa hilo.

Kwa mujibu wa Zakayo Kalebo meneja wa uhusiano wa jamii wa kampuni hiyo idadi ya nyumba imeongezeka na pikipiki zimejaa na kimsingi watu wanauona mgodi huo kuwa na manufaa kwa sababu maendeleo makubwa yameweza kufikia hali ambayo haikuwa hivyo kabla ya kuwepo kwa mgodi huo.

David amehamia Mara Kaskazini kutoka Kenya David amehamia Mara Kaskazini kutoka Kenya

Kusema kwamba hali hiyo imesaidia kukuza uchumi au kusema ni neema ya mali ghafi itakuwa kama ni kutia chumvi kwa Mara Kaskazini. Biashara ya dhahabu huwavutia watu wengi kutoka nje. Kwa mfano David Arumba aliigia hapo mwaka uliopita kutoka nchi iirani ya Kenya ana umri wa miaka 25 ni mtu pekee katika familia yake aliekwenda shule. Lakini haafiki kufanya kazi za uvamizi na ameamuwa kuwa na kazi tafauti. Anasema watu wengi wanaokwenda hapo huishia kupigwa risasi na wengine kujeruhuiwa.

Yeye hakutaka kuwa kwenye matatizo ya kufukuzana na polisi na kuwepo mahala ambapo hakustahiki.Ameamua kuwa na biashara ya kuosha magari kwa kuwa inampa uhuru.

Kijana huyo ana sehemu ndogo ya kuosha magari katika kijiji cha Kewanja na mke wake humsaidia kwa kuuza ndizi na mafuta ya petroli katika chupa za plastiki.Wengi ya wanavijiji hao wanaishi kwa kutegemea pungufu ya dola moja kwa siku na kuweza kuwa na maji na umeme ni vitu vya anasa.

Nini tatizo Mara Kaskazini ?

Sospeter Muhongo ni waziri wa madini wa Tanzania mwenyewe anatoka Mara Kaskazini ni mwanaeleojia na amekuwa katika wadhifa huo kwa miezi kadhaa. Ameongeza kodi kwa kampuni hizo na amekuwa akitaka zijihusishe zaidi na miradi ya kusaidia jamii.Muhongo anasema wamejaribu na hawatosita watafanya juhudi zote kuhakikisha kwamba kuna amani na usalama katika eneo hilo. Anaona njia moja ya kulitatua tatizo hilo ni kuwekeza katika elimu ambapo watu watakapokuwa wamejifunza na kuelimika vizuri watakuja kuwa na fikra tafauti.

Elimu ni ufumbuzi Waziri Sospeter Muhongo "Elimu ni ufumbuzi" Waziri Sospeter Muhongo

Lakini hadi sasa hakuna ishara ya kuwa na fikra tafauti katika kijiji cha Kewanja mkoa wa Mara Kaskazini. Biashara hiyo haramu ya dhahabu hufanyika kwa vificho na mawe kuvunjwa vipande vipande kuichuja dhahabu huko vijijini. Juu ya kwamba utaratibu wa kuisafisha dhahabu hiyo huhusisha matumizi ya zebaki ambayo ni hatari kwa afya lakini hivyo ndivyo anavyofanya Jumanne ambaye anasema binaadamu lazima atambuwe wapi anaweza kupata riziki yake kwani fedha anazoweza kupata kwa siku moja inabidi asubiri kwa mwaka mzima kuweza kuzipata akijishughulisha na kilimo.

Kidonge cha dhahabu kinachong'ara kwenye mkono wake pengine hakizidi hata gramu moja. Huuzwa kwa Euro 20 kwenye soko la magendo. Ni sehemu ndogo ya utajiri wa mali ghafi lakini ni fedha nyingi kwa maskini walioko kaskaziini mwa Tanzania.

Mwandishi: Julia Hahn/Mohamed Dahman

Mhariri:Yusuf Saumu

SOURCE:DW.DE

Je, ndio machweo ya chama kongwe cha Tanzania?

 Bendera ya Tanzania

Watanzania wanataka kutunga katiba itakayoongoza nchi yao bila kuwepo haja ya kufanya marekebisho. Lakini baadhi ya wanasiasa wanasemekana kuwa wameanza kampeni kutafuta nafasi za uongozi bila idhini.

Lakini suala kubwa katika vichwa vya raia ni kama sheria mama ya nchi inayoandaliwa sasa italeta mabadiliko bora zaidi au itaiweka nchi katika kibano cha watu wasiopenda mabadiliko, ambao tayari wameanza kutamka kuwa wanapinga mabadiliko yaliyo katika rasimu ya katiba.

  Mfuasi wa CCM Zanzibar

Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaonekana kuwa bado ni maarufu katika baadhi ya jamii na kinapendwa kiendelee kutawala angalau kwa mwongo mmoja zaidi, lakini ukweli ni kwamba wimbi la upinzani kuhusu pingamizi zake kwa mawazo mapya linainuka zaidi. Hapana shaka hakiwezi kutawala milele.
Muda, nyenzo, fedha na raslimali watu mara nyingi vimekuwa haba kuwawezesha Watanzania watekeleze mipango na malengo yao kwa ukamilifu.
Kwa mfano, takwimu za watu zilizopo sasa ni makadirio yaliyotokana na sensa ambayo haikukamilika ya mwaka 2012 ambayo iliacha wakazi wa maeneo yasiyofikika kwa urahisi bila kurekodiwa katika orodha za makarani wa sensa.
Sababu hiyo hiyo ya kutofikika kwa maeneo hayo bado ni kikwazo katika harakati za sasa ambazo zinahitaji wananchi wote washiriki kikamilifu, ikiwa pamoja na utoaji wa maoni yao katika maboresho ya rasimu ya katiba mpya.

Kutunga katiba upya na kuandaa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ni shughuli za gharama kubwa na hapana budi zikamilishwe katika kipindi cha miaka miwili kwa kuzingatia haki kwa raia wote na kwa njia ya kidemokrasia.

CCM yaamini itashinda 2015

Kweli Tanzania imefika mahali pagumu katika historia yake. Watu wake lazima wauthibitishie ulimwengu kwamba bado wameungana na wanauenzi muungano wa karibu nusu karne kati ya Bara, eneo ambalo lilijulikana kama Tanganyika, na Visiwa vya Zanzibar, hasa ya mawazo tofauti kuhusu siku zijazo za muungano baada ya kutangazwa kwa rasimu ya katiba.

  Rais wa kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere

Huo ni upande mmoja wa hali ya kisiasa katika nchi hii ya Julius Kambarage Nyerere na Abeid Amani Karume, waasisi wa taifa la Tanzania. Upande mwingine, ingawa hakuna hakika ya nani atakuwa mshindi katika kura ya maoni juu ya katiba mpya, kila chama cha siasa na washabiki wake wanachukua tahadhari wasije wakajiangamiza wenyewe kwa jinsi wanavyoendelea na harakati za sasa.

Matokeo ya katiba mpya huenda yakawa na athari kwa maendeleo yao katika uwanja wa siasa, lakini pia muonekano wao kama viongozi makini, wanaoaminika na wenye upeo mbele ya vijana ambao idadi yao inazidi kuongezeka. CCM inaamini kuwa itaibuka na ushindi mkubwa 2015, lakini kama matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni katika kata nne za jiji la Arusha ni kielelezo cha yajayo, basi chama kianze kufikiria kuachia ngazi kwa heshima.

Kwanini CCM inapinga serikali tatu?

Bendera ya chama cha upinzani CUF  

 Bendera ya chama cha upinzani CUF

Washindani wake wa karibu, CHADEMA na Chama cha Wananchi (CUF), wanakipa taswira ya kuwa kiko ukingoni mwa mteremko mkali – licha ya hayo yanayoelezwa kuwa "mafanikio ya CCM’" katika historia ya Tanzania. Upingaji wa sera za CCM uko zaidi miongoni mwa kizazi cha vijana ambao shauku zao zaidi ni kuhusu ajira, elimu ya utaalamu katika nyanja mbalimbali na ya ufundi stadi, uhuru wa kijamii na maisha bora kuliko musuala ya uwakilishi bungeni na katika serikali za mitaa.

Kwa mawazo yao, baadhi ya vijana wanasema, CCM ni chama cha watu wanaotafuta nafasi za kujinufaisha wao binafsi bila kujali watu wengine ; na watu ambao kila mara huzungumzia harakati za ukombozi wa Afrika wakati wao wanahitaji ukombozi wa kifikra.

Wadadisi wanauliza, kwa mfano, kwa nini CCM inapinga kuwepo kwa serikali tatu za Tanganyika, Zanzibar na Muungano ambao ndio mfumo unaotakiwa na raia wengi.
Wachambuzi wa kisiasa wanaongeza kuwa kukataa mfumo wa serikali tatu kama rasimu ya katiba inavyopendekeza ni kuhujumu Muungano wa Tanzania. Wana wasiwasi kwamba huenda chama kina dondoo ya siri, lakini katika enzi hizi za uwazi, ni Watanzania wachache wanaweza kurubuniwa na chama ambacho kinaelekea kuishiwa ujanja wa kisiasa kuvutia watu wengi wakiunge mkono.

Mwandishi: Anaclet Rwegayura

Mhariri: Josephat Charo

SOURCE:DW.DE