Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristu, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuwekwa Wakhfu Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, iliyofanyika jijini Mwanza jana.
Monday, 20 October 2014
Makamu wa rais mgeni rasmi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristu, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuwekwa Wakhfu Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, iliyofanyika jijini Mwanza jana.
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO

Simu ya Upepo : “N G O M E” Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo : DSM 22150463 Sanduku la Posta 9203,
Telex : 41051 DAR ES SALAAM, 20 Octoba, 2014
Tele Fax : 2153426
Tovuti : www.tpdf.mil.tz
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania
(JWTZ) linatoa taarifa kwa wananchi wote kuwa ni kosa kisheria kumiliki
au kuvaa sare za JWTZ kwa mtu yeyote asiyehusika.
Aidha, kumeonekana matukio
kadhaa ya baadhi ya vikundi, ama mtu mmoja mmoja kumiliki au kuvaa sare
za JWTZ. Inakumbushwa kuwa kwa yeyote atakayeonekana amevaa ama
kumiliki sare hizo sheria itachukua mkondo wake.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0783 - 309963
Monday, 13 October 2014
KUMBUKUMBU YA MIAKA 15 TANGU KIFO CHA MWALIMU NYERERE
WATANZANIA leo tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka 15 tangu kufariki kwa muasisi na Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mwalimu Nyerere alifariki dunia Oktoba 14, 1999 akiwa nchini Uingereza alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya kansa ya damu.
Akizindua rasmi maadhimisho ya kumbukumbu hizo jana, Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Kate Kamba alisema kitaifa maadhimisho hayo yatafanyika mkoani Tabora
Saturday, 17 August 2013
Pistorius to go on trial in March
Star South African sprinter Oscar Pistorius will go on trial in March next year on murder charges for shooting his girlfriend, his lawyer said Saturday.
"The trial will be in March next year. It will be from the first week of March until end of March," attorney Kenny Oldwage told AFP.
On Monday, the 26-year-old double-amputee sprinter is to appear in the Pretoria Magistrate's Court, where he is expected to be served with an indictment for murdering girlfriend Reeva Steenkamp in the early hours of Valentine's Day.
He claims he shot Steenkamp through a locked bathroom door of his upscale home because he mistook her for an intruder.
The state is arguing that the murder was premeditated, a charge which carries a sentence of life imprisonment.
Oldwage refused to comment on local media reports that Pistorius may face two new charges related to firing a gun in public when he appears in court next week.
According to eNCA television news, one of the charges is linked to an event in January when Pistorius accidentally fired a gun in an upmarket Johannesburg restaurant.
In another case, Pistorius allegedly discharged his gun out of the sunroof of a friend's car on their way back from a holiday.
Paralympic champion Pistorius, who was born without calf bones and had both legs amputated below the knee when he was 11 months old, runs on fibre-glass prosthetic legs.
He catapulted to fame at last year's London Olympics as the first double-amputee to compete against able-bodied athletes.
SOURCE:AFP
Mwakyembe aagiza wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wakamatwe!
Ni Koplo Ernest, Yusuph, Jackson, Juliana Tadei na Mohamed.
Aidha, amesema wafukuzwe mara moja ni baada ya kupitia CCTV na kuona namna walivyohusika siku hiyo kwani walionekana wakipiga simu mara watoke nje kinyume na sheria za chumba cha ukaguzi (vifaa hivi ni kama vilivyotumika na CHADEMA kuwanasa polisi waliorusha bomu na baadae kuwashambulia kwa risasi).
Hao waliotajwa hapo juu ni waliofanikisha kupitisha kilo 180 zilizokuwa zimebebwa na wasichana wawili (Masogange na mwenzake) waliokamatwa huko Afrika kusini..
Aidha, amesema wafukuzwe mara moja ni baada ya kupitia CCTV na kuona namna walivyohusika siku hiyo kwani walionekana wakipiga simu mara watoke nje kinyume na sheria za chumba cha ukaguzi (vifaa hivi ni kama vilivyotumika na CHADEMA kuwanasa polisi waliorusha bomu na baadae kuwashambulia kwa risasi).
Hao waliotajwa hapo juu ni waliofanikisha kupitisha kilo 180 zilizokuwa zimebebwa na wasichana wawili (Masogange na mwenzake) waliokamatwa huko Afrika kusini..
ANC kususia ibada ya Marikana
Maelfu ya raia wa Afrika Kusini wamekusanyika katika mgodi mkubwa wa dhahabu nyeupe kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuuawa kwa wachimba migozi 34. Chama tawala cha ANC kimesema hakitahudhuria makumbusho ya leo kikisenya yanatumiwa kukejeli utawala wa nchi.
Katika maadhimisho hayo Afisa mtendaji wa kampuni ya, Lonmin, Ben Magara amwaomba mshamaha familia za wachimba migodi 34 waliouawa.
Tofauti kati ya makundi mawili ya vyama vya wafanyikazi zililaumiwa kwa kuzuka vurugu zilizotokea mwaka jana.Chama kilicho na uhusiano wa karibu na ANC- National Union Of Mineworkers kimepingwa na wachimba migodi wengi na kuanzisha chama kipya. Mauaji hayo yalisababisha gathabu ya umma na kupelekea lalama nyingi dhidi ya sekta ya madini.
Afrika Kusini ina asili mia 80 ya madini ya dhahabu na dhahabu nyeupe.Mauaji ya wafanyikazi hao yalitajwa kuwa mabaya zaidi tangu kumalizika kwa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini mwaka 1994. Sherehe za leo zimepangwa na chama kipya cha kutetea maslahi ya wachimba migodi Mineworkers and Construction Union (Amcu) ambacho kinashinikiza nyongeza zaidi ya marupurupu ya wafanyikazi.
AMCU ndicho kikubwa zaidi katika mgodi wa dhahabu nyeupe inayomilikiwa na kampuni ya Lonmin.Baadhi katika chama tawala cha ANC wameelezea hofu huenda chama hicho kikaungana na aliyekua kiongozi wa vijana Julius Malema ambaye alifukuzwa chamani kwa makosa ya nidhamu.
Malema ameunda chama chake cha kisiasa. Rais Jacob Zuma aliunda tume ya kuchuguza matukio yaliyopelekea mauaji ya wachimba migodi hio. Mwandishi wa BBC Afrika Kusini anasema kumekuwa na ghathabu ya umma kwani hadi sasa hakuna polisi hata mmoja aliyewajibishwa na mauaji hayo.
CHANZO:BBC
Maelfu wajitokeza kuandamana tena Misri
Maelfu ya wafuasi wa Rais wa Misri aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi wameanza maandamano mengine mjini Cairo, huku kukiwa na hofu ya kuzuka makabiliano zaidi. Maafisa wa usalama wamezingira barabara kuelekea medani ya Ramses ambapo maandamano hayo yalipangwa kufanyika. Maandamano ya sasa yanajiri siku mbili baada ya jeshi kuvunja kambi ambapo wafuasi wa vuguvugu la Muslim Brotherhood walikua wamesalia kwa zaidi ya mwezi mmoja.
Makabiliano yalizuka na zaidi ya watu 600 wakauawa, maelfu walijeruhiwa.Maandamano zaidi yanaendelea nje ya mji mkuu Cairo na taarifa zinasema watu wanne wameuawa kwenye makabiliano eneo la Ismailia. Polisi wa Misri wameamrishwa kutumia risasi za moto kulijinda na kulinda majengo ya serikali dhidi ya kushambuliwa.
Huku utawala wa mpito ukitangaza hali ya
hatari, mwandishi wa BBC aliyeko Cairo amesema taharuki imetanda mji
mzima.Maelfu walikusanyika nje ya msikiti mmoja baada ya Muslim
Brotherhood kuwaomba wafuasi wao kuandamana baada ya sala ya ijumaa
wakiitaja kama siku ya hasira.
Magari ya kijeshi yanashika doria mjini Cairo, na njia ya kuingia medani ya Tahir kitovu cha maandamano ya mwaka 2011 yaliyomuondoa madarakani Hosni Mubarak imefungwa. Huku haya yakiarifiwa wapinzani wa Mohammed Mosri pia wamepanga kuandamana dhidi ya mahasimu wao. Wakati huo huo watu wameombwa kulinda makaazi yao, makanisa na biashara. Wakristo nchini Misri wamekuwa wakilengwa katika siku za karibuni na makundi ya kiisilamu yenye misimamo mikali. Jumla ya makanisa 25, makaazi na biashara yalishambuliwa hapo Jumatano na Alhamisi.
chanzo;BBC
Subscribe to:
Posts (Atom)