Wacheza soka Nigeria wapigwa marufuku
 Wachezaji na maafisa wa vilabu waliohusishwa na kupanga mechi ambazo 
hatimaye zilimalizika kwa mabao 79-0 na 67-0 wamepigwa marufuku maisha
Wachezaji na maafisa wa vilabu waliohusishwa na kupanga mechi ambazo 
hatimaye zilimalizika kwa mabao 79-0 na 67-0 wamepigwa marufuku maisha
Kilabu cha Plateau United Feeders walishinda mchuano wako kwa mabao 
79-0 dhidi ya kilabu cha Akurba FC wakati kilabu cha Police Machine FC 
kilipoibwaga Bubayaro FC kwa mabao 67-0.
                     
Vilabu hivyo vimepigwa marufuku kushiriki michauno yoyote kwa miaka 10.
                     
Kamati moja ya Shirikisho la soka la Nigeria 
ilipendekeza kuwa maafisa wa soka waliohusika katika upangaji huo wa 
michuano miwili kupigwa marufuku maisha.
                     
Plateau United Feeders na Police Machine 
waliingia kwenye mechi yao wakiwa na pointi sawa huku wakiwa katika 
hatari ya kuvuka na kuingia daraja ya chini ya ligi ya kitaifa ikiwa 
wangepoteza mechi .
                     
Feeders ilishinda kwa mabao 72 katika kipindi 
cha pili cha mechi, wakati Police Machinen nao wakipata mabao 61 baada 
ya kipindi cha mapumziko.
                     
Matokeo hayo yalimaanisha kuwa Plateau ilipanda daraja juu ya Police Machine kwa toafuti ya mabao.
                     
Shirikisho la soka Nigeria limesema kuwa limekubali mapendekezo hayo na kuwa litawasiliana na vilabu husika, pamoja na FIFA.
                     
Shirikisho hilo lilisema litachapisha majina ya wachezaji , picha zao na maelezo kuwahusu.
CHANZO:BBC SPORT 
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment