Rais mstaafu wa Nigeria Olesegun Obasanjo yuko 
nchini Zimbabwe kama mwangalizi wa uchaguzi mkuu
Kampeini za kisiasa nchini Zimbabwe zinamalizika hii leo kabla ya uchaguzi mkuu hapo Jumatano wiki hii.
                     
Kiongozi wa chama cha Movement for Democratic 
Change ambaye pia ni Waziri MKuu ,Morgan Tsvangirai, hii leo atahutubia 
mkutano wa hadhara mjini Harare katika uwanja alikofanya mkutano wake 
hio jana Rais Robert Mugabe.
                     
Viongozi hao wawili wamekua katika serikali ya 
muungano tangu mwaka wa 2008 na wametofautiana kuhusu muda uliowekwa 
kufanyika uchaguzi. Kumekua pia na madai ya wizi wa kura, na vitisho 
dhidi ya wafuasi wa MDC.
                     
Shirika la kimataifa linalotathmini hali ya 
mizozo The International Crisis Group limeonya kwamba hakuna mazingira 
ya uchaguzi huru na haki Zimbabwe.
BBC 
 
No comments:
Post a Comment