Maandamano yafanyika nchini Tunisia
 
 
           Mohamed Brahmi 
Tunisia inashuhudia mgomo wa taifa zima baada ya kuuawa kwa kiongozi wa upinzani Mohamed Brahmi.
                     
Chama cha wafanyakazi kikubwa kuliko vyote 
nchini Tunisia, UGTT, kimetoa wito wa kuwataka wananchi kupinga "ugaidi,
 ghasia na mauaji".
                     
Alhamisi polisi walitumia mabomu ya kutoa 
machozi kuwatawanya waandamanaji katika miji kadhaa nchini humo, baada 
ya Bwana Brahmi kuuawa kwa kupigwa risasi nje ya nyumba yake mjini 
Tunis.
                     
Chama tawala nchini Tunisia, cha Kiislam cha 
Ennahda kimekanusha tuhuma kutoka kwa ndugu wa marehemu kuwa kilikula 
njama katika mauaji ya Bwana Brahmi.
SOURCE:BBC 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment