After years of dilly-dallying and secrecy by the government on who owns
much cash in offshore accounts, the Alliance for Change and Transparency
(ACT-Wazalendo) party will finally reveal the names of those involved
on July 4.
But Attorney General George Masaju who revealed in February that the
report on the same matter was ready and that it would be tabled in
Parliament chose to keep mum when The Citizen demanded to know when it
would be presented as the House’s life comes to an end on July 9.
President Jakaya Kikwete is expected to address the National Assembly on
July 9 and later dissolve Parliament to pave the way for the country’s
General Election slated for October 25.
Yesterday, ACT-Wazalendo party leader Zitto Kabwe told a news
conference, barely a day after he completed his tour of different
regions, that he would provide a list of 99 bigwigs behind the Swiss
Billions at a public rally.
Mr Kabwe and other party leaders had for the last three weeks been
traversing various regions to popularize the party and the newly
launched Tabora Declaration which seeks to revive the now defunct Arusha
Declaration.
Addressing a news conference, Mr Kabwe said on July 4, the party will
hold a huge political rally at Mwembeyanga grounds in Dar es Salaam
where he would reveal the names of people with ofshore accounts in the
and the amount of cash they had stashed.
The ACT-Wazalendo party’s move comes at a time when a big cloud still
hangs over the ‘Swiss Billions’ even as Mr Masaju made a revelation that
the report of a taskforce led by the Prevention and combating of
Corruption Bureau (PCCB) director general Edward Hosea was ready.
Mr Hosea revealed in February, just few days after he was appointed AG,
to succeed former AG, Judge Fredrick Werema, who resigned following the
Tegeta escrow account scandal.
Addressing editors in Dar es Salaam at his maiden press conference, Mr
Masaju said the final report would be tabled in Parliament any time. He
stressed that Parliament would then debate the document and decide on
the next course of action.
However, almost five months down the line, the report has been shelved
and the government is still silent. At Parliament grounds in Dodoma, the
AG appeared to run away from questions on the controversy surrounding
the matter. When asked by The Citizen to give any statement on the
promise he made before editors in February, the AG said: “I cannot
comment on that issue because everything here depends on Parliament’s
schedule.
The Citizen further sought comment from Deputy Speaker of the National
Assembly Job Ndugai concerning the ‘Swiss Billions’ report, but MrNdugai
said his office was yet to receive it.
“We understand this matter was being pushed by the former Kigoma North
MP, but as of today the government is yet to bring the report to the
office of the Speaker and I think you should contact the AG,’’ he said
Wednesday, 1 July 2015
Tuesday, 30 June 2015
US Gay Marriage: Robert Mugabe Asks Obama to Marry Him
Zimbabwean president Robert Mugabe has challenged US President Barack Obama by asking his hand in marriage. His comment comes at the back of the legalization of gay marriage in the US by the Supreme Court.
During Mugabe's weekly radio interview with Zimbabwe’s national radio last Saturday, he said:
“I’ve just concluded since President Obama endorses the same-sex marriage, advocates homosexual people and enjoys an attractive countenance thus if it becomes necessary , I shall travel to Washington, D.C. , get down on my knee and ask Obama’s hand. I can’t understand how these people dare to defy Christ’s explicit orders as our Lord prohibited mankind from sodomy.''
Mugabe said the American Government is run by pervert, Satan-worshipers who insult the Great American nation.
He reportedly added
"That the American tradition and heritage was based on lofty Christian principles, but to the detriment of this great nation, America’s corrupt political elite is acting according to their diabolic whims.
Obama’s endorsement of gay marriage, the first ever from a sitting president, came amid growing pressure for the president to clarify his previously muddled opinion.
Obama’s endorsement of gay marriage, the first ever from a sitting president, came amid growing pressure for the president to clarify his previously muddled opinion, as two senior members of his administration announced personal support for gay marriage and a day after voters in North Carolina approved a state constitutional amendment defining marriage as a union between a man and a woman.
Source: awdnews.com
Kumekucha: Mwinyi, Mkapa, Aman Abeid Karume Wakutana Rasmi Kuwajadili Wagombea Urais Wa CCM
Hatimaye marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa wameungana na wajumbe wenzao wa Baraza la Ushauri la Wazee wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanza kuwajadili makada waliojitokeza kuwania urais na kutoa ushauri utakaowezesha kupatikana kwa njia bora za kumpata mgombea wa chama hicho.
Tayari vikao vya baraza hilo vilivyokuwa vikisubiriwa kwa hamu vimeshaanza na leo vinaingia katika siku yake ya tatu, kwenye ofisi moja nyeti jijini Dar es Salaam.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya baraza la wazee hao zinaarifu kuwa vikao hivyo vina umuhimu wa pekee katika mchakato huo na kwamba vimepewa eneo tulivu na lenye usalama wa hali ya juu.
"Kikao kimeanza hapa (anataja ofisi) tangu juzi (Jumamosi) na hivi sasa bado tunaendelea,” kilieleza chanzo kimoja toka ndani ya kikao hicho.
Katika hali inayoonyesha umuhimu wa ushauri wa baraza hilo, chanzo hicho kinasema, “tuombe Mungu ili yanayoazimiwa na wazee wetu yakamilike na kuweza kukipa sura mpya chama chetu (CCM).”
Hata hivyo, taarifa nyingine kutoka ndani ya CCM zinaeleza kuwa hivi sasa baraza hilo linapewa umuhimu mkubwa kutokana na hali ya ‘mnyukano’ unaowahusisha wanasiasa wakongwe wakiwamo waliotegemewa kutoa ushauri ili kivuke salama katika mchakato unaohusu Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25 ili hatimaye apatikane mrithi wa Rais Jakaya Kikwete kwa nafasi ya urais na uenyekiti wa CCM.
Awali, kikao cha wazee hao kilikuwa kifanyike Jumatano iliyopita lakini kiliahirishwa na katibu wake, Pius Msekwa, kutokana na kile alichokieleza kuwa ni baadhi ya wajumbe kuwa safarini.
Wazee hao, pamoja na mambo mengine kuhusiana na uchaguzi, wanakutana kujadili mwenendo wa mbio za urais ndani ya CCM ikiwa ni siku chache kabla ya kufikia Julai 2, mwaka huu, ikiwa ni siku ya mwisho ya kurejesha fomu kwa wanaowania urais kupitia chama hicho.
Hadi kufikia jana, makada 42 wa chama hicho walijitokeza na kuchukua fomu za kuwania kuteuliwa kuwa wagombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25.
Mbali na marais wastaafu Mwinyi na Mkapa, wengine wanaounda Baraza la Ushauri la Wazee kwa mujibu wa mabadiliko yaliyofanywa na CCM mwaka 2012 katika katiba yake ni marais wastaafu Mwinyi (Mwenyekiti), Mkapa (Mjumbe), Amani Abeid Karume (Mjumbe) na Dk. Salmin Amour (Mjumbe).
Wengine ni Waziri Mkuu mstaafu na Makamu wa Kwanza wa Rais, John Malecela (mjumbe) na Pius Msekwa (Katibu).
Credit: Nipashe
Zitto: Sitagombea Urais wala Ubunge 2015
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema hafikirii kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho wala ubunge katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Alisema mwaka 2015, ndio mwaka wa mwisho kujihusisha na siasa ambapo dhamira yake ni kutafuta chuo ambacho ataweza kufundisha masomo ya uchumi na maliasili.
Bw. Kabwe aliyasema hayo hivi karibuni katika mahojiano maalumu na gazeti hili siku chache baada ya viongozi 105 kutoka Vyuo Vikuu 30 nchini, kupendekeza majina ya wanasiasa wanaofaa kuwania urais mwaka 2015.
Jina la Bw. Kabwe, lilishika nafasi ya pili katika mchujo huo ambapo Mbunge wa Bumbuli, mkoani Tanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Bw. January Makamba, alishika nafasi ya kwanza kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwanasiasa aliyeshika nafasi ya tatu katika mchujo huo alikuwa Mbunge wa Ubungo, Dar es Salaam, Bw. John Mnyika (CHADEMA).
"Hiki ni kipindi cha mwisho kwangu kujihusisha na siasa kwani nimechoka nazo, nitatafuta chuo nikafundishe na kama nitakosa ni bora nikalime michikichi... sihitaji urais," alisema.
Katika mkutano wa wanafunzi hao, walisema Bw. Makamba ana sifa zote za kuwa rais wa nchi kamaatagombea nafasi hiyo mwaka 2015 ili aweze kulikomboa Taifa ambalo hivi sasa linakabiliwa na matukio mengi ya uvunjifu wa amani.
Wanafunzi hao walikwenda mbali zaidi na kuyataja baadhi ya matukio hayo kuwa ni pamoja na vurugu, kutekwa kwa watu wasio na hatia, kufanyiwa vitendo vya ukatili, kumwagiwa tindikali na kupungua kwa mtangamano wa kijamii.
Mwenyekiti wa mkutano huo ambao ulifanyika mkoani Morogoro ambaye pia ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Kampasi ya Mbeya, Bw. Theonest Theophil, alisema Bw. Makamba alipata kura 72 ambapo Bw. Kabwe alipata kura 20.
Bw. Theophil alisema sifa za kiongozi wanayemtaka kwanza awe kijana mwenye fikra mpya, atakayeleta matumaini mapya, kuwaunganisha Watanzania, asiyeendekeza siasa za kikanda, mdini na mkabila.
Sifa nyingine ni kiongozi mwadilifu asiye na rekodi ya kutuhumiwa mahali popote kwa vitendo viovu, mtulivu, mwenye busara na anayepima kauli zake.
Source: Majira
Maelezo ya Bernard K. Membe, Kuhusu Fedha za Deni la Libya
1.0. Libya ni moja kati ya nchi wafadhili
wa Tanzania ambapo, kama ilivyo wafadhili wengineimekuwa ikiipa nchi
yetu misaada na mikopo yenye masharti nafuu. Serikali yetu imekuwa
ikifanya taratibu mbalimbali kulipa madeni ya nchi wafadhili kwa njia
mbalimbali ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kubadili madeni na kuyaingiza
katika miradi n.k, yaani ‘Dept Swap’.
2.0. Katika utaratibu huo wa ‘Dept Swap’, tarehe 20/7/2005, Serikali ya Tanzania na Libya zilitia sahihi mkataba wa Dept Swap (Dept Swap Agreement) ambao uliweka utaratibu wa matumizi na urejeshaji wa fedha za deni la Libya.
3.0. Tarehe 4/3/2009, Serikali ya Libya na Tanzania zilitia sahihi mkataba wa nyongeza (Addendum to the Dept Swap Agreement) ambao ulizungumzia, pamoja na mambo mengine, matumizi ya jumla ya dola za Kimarekani milioni 20 (20,000,000) ambazo zilikuwa zimehifadhiwa katika akaunti ya Libya No.004-200-0002216-01, Benki ya Rasilimali Tanzania (Tanzania Investment Bank).
4.0. Nyongeza hii ya mkataba ilitamka bayana katika kifungu No.4.02, kwamba, fedha zilizokuwa katika akaunti tajwa, zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua wao wenyewe, ambaye ni kampuni ya MEIS INDUSTRIES LIMITED kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha Saruji Lindi. Kwa mujibu wa nyongeza hii, mkopo ulipaswa kulipwa ndani ya miaka sita, na baada ya hapo, fedha hizo zirejeshwe na ziendelee kukopeshwa Watanzania kwa ajili ya miradi mingine ambayo Serikali za Libya na Tanzania zitakuwa zimeridhia.
5.0. Kumbukumbu zinaonyesha mambo mawili:-
5.1 Kwamba, kabla ya Serikali ya Libya kutia sahihi nyongeza hii ya mkataba iliyotaka fedha zikopeshwe kwa MEIS INDUSTRIES, upembuzi yakinifu wa mradi husika ulifanywa na serikali ya Libya kupitia vyombo vyake, na wao wenyewe walishajiridhisha juu ya ubora wa mradi huo (Viability of the Project)
5.2 Kwamba, baada ya kutia sahihi nyongeza ya mkataba, Serikali ya Libya kupitia Ubalozi wake hapa nchini iliendelea kusisitiza kwa maandishi kwamba Serikali ya Tanzania iharakishe mchakato wa kuwezesha fedha hizo zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua ili mradi huo muhimu usiendelee kuchelewa, na pia fedha ziingie katika mzunguko kwa manufaa ya Watanzania.
6.0. Katika kutekeleza mikataba hii miiwli, yaani Dept Swap Agreement ya tarehe 20/7/2005 na Addendum Dept Swap Agreement ya Tarehe 4/3/2009, na kwa kuzingatia umuhimu ambao serikali ya Libya iliuonyesha, Serikali ya Tanzania kupitia watalaamu wake wa Wizara ya Fedha, Benki ya Rasilimali (TIB) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, na Mwekezaji (Kampuni ya MEIS), walikutana chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na kuandaa hadidu za rejea ambazo zilipelekea kutengenezwa kwa mkataba wa uwekezaji (Investment Agreement) kati ya serikali ya Tanzania, TIB, Serikali ya Libya na Mwekezaji.
7.0. Serikali ya Tanzania, TIB na Mwekezaji walitia sahihi mkataba huu na kuupeleka Libya ili serikali ya Libya ipate kuweka sahihi. Kwa sababu ambazo hazikufahamika, serikali ya Libya haikutia sahihi mkataba huo.
8.0. Baada ya kufuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio, mwekezaji alimuandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania yenye kumbukumbu No. PC/MEIS/AG/2/10 ya tarehe 1/9/2010 akieleza kusudio la kuipeleka Serikali ya Libya Mahakamani kwa kitendo chake cha kutokutia sahihi mkataba.
9.0. Terehe 13/9/2010, Mwekezaji alifungua shauri Mahakama Kuu ya Tanzania, shauri la madai No. 124/2010 dhidi ya serikali ya Libya, akiiomba Mahakama Kuu itoe tamko kwamba kitendo cha serikali ya Libya kukataa kutia sahihi mkataba huu hakikuwa kitendo cha haki na kwamba mahakama itoe amri kwamba fedha hizo zitolewe kwa Mwekezaji ili kutekeleza mradi uliokusudiwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba wito wa Mahakama (Summons) ulipelekwa Ubalozi wa Libya lakini hapakuwa na majibu wala mwakilishi aliyekuja mahakamani.
10.0. Mahakama Kuu, kwa kufuata taratibu zake, iliendelea na kusikiliza shauri na kutoa amri kama ambavyo mahakama yenyewe ilijiridhisha. Amri ya mahakama, pamoja na mambo mengine, iliagiza kwamba fedha hizo zitolewe kwa mwekezaji ili kutekeleza mradi husika.
11.0. Zilifanyika juhudi za Benki ya Rasilimali (TIB) pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupinga au kupata ufafanuzi zaidi juu ya amri hiyo ya utekelezaji wake. Mahakama Kuu pamoja na Mahakama ya Rufana, katika nyakati tofauti, zilishughulikia maombi hayo na kuyafikisha katika hatima yake kwa mujibu wa sheria. Kwa ajili ya kumbukumbu, mashauri yaliyofunguliwa ni kama ifuatavyo:-
11.1 TIB ilifungua maombi No. 126/2010 katika mahakama ya Rufaa kuiomba izuie na kufuta utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu. Maombi haya ya TIB yalifanyiwa uamuzi wa mwisho mnamo tarehe 7/11/2011, ambapo maombi hayo yaliondolewa mahakamani kwa kuwa, kwa mujibu wa Mahakama ya Rufaa, hayakuwa yamefuata taratibu za kisheria.
11.2 Mwanasheria Mkuu wa Serikali naye akapeleka maombi Mahakama ya Rufaa. Maombi ya kwanza, maombi namba .146/2010 akiomba Mahakama ya Rufaa kufuta mwenendo mzima wa kesi pamoja na amri ya Mahakama Kuu, na maombi ya pili No. 147/2010 ikiiomba Mahakama ya Rufaa izuie utekelezaji wa amri ya mahakama Kuu (Stay of Execution). Maombi haya yote yalisikilizwa na kuamuliwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za kimahakama.
12.0 Wakati haya yakiendelea, ilijitokeza kampuni ya Mohamed Enterprises Limited ikidai kwamba ina haki juu ya fedha hizi. Nayo ikafanya yafuatayo:-
12.1 Ilipelea maombi Mahakama Kuu kuzuia utekelezaji wa hukumu kwa madai kuwa kampuni hiyo nayo ilikuwa ikiishtaki Serikali ya Libya katika kesi ya madai No. 110/2010 na kwa hiyo, endapo amri ya Mahakama Kuu ingetekelezwa kwa kumpa mwekezaji (Kampuni ya MEIS) fedha za Libya, basi wao (Mohamed Enterprises Limited) wangekosa mahali pa kutekeleza/kukazia hukumu waliyokuwa wakiitarajia katika kesi yao (no. 110/2010) dhidi ya serikali ya Libya. Maombi haya yalisikilizwa na Mahakama Kuu na kutolewa maamuzi stahiki.
12.2. Kampuni ya Mohamed Enterprises Limited haikuridhika na uamuzi wa Mahakama Kuu kwa hiyo kapeleka shauri hili Mahakama ya Rufaa, kupitia maombi (Civil Revision) No. 2/2011. Maombi haya nayo pia yalisikilizwa na kutolewa maamuzi.
13 Mwisho wa yote maamuzi ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa katika mchakato mzima yakawa kwamba mwekezaji (Kampuni ya MEIS) alikuwa na haki ya kupewa fedha za mradi wa Kiwanda cha Saruji Lindi kama ilivyoanishwa katika mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Libya. Ni dhahiri kwamba, mgogoro huu ulichujwa na mahakama mpaka ngazi ya juu kabisa, tena kwa nyakati tofauti na mbele ya waheshimiwa majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.
14.0 Katika Taifa linaloongozwa kikatiba, chini ya utawala wa sheria kama Tanzania, ambapo Mahakama ndicho chombo kilichopewa mamlaka ya mwisho kuamua juu ya haki za raia na hata serikali, si rahisi na wala haitakuwa sahihi kwa mtu yeyote kuhoji uhalali wa mchakato huu kama ulivyoongozwa, kuelekezwa na kuamuliwa na mahakama, isipokuwa tu kama sheria inatoa mwanya mwingine kurudi mahakamani kwa mtu yeyote ambaye hajaridhika au anayetaka kuhoji maamuzi haya kwa namna yoyote.
15. Mahakama iliamua kwa mujibu wa sheria. Na kwa kuwa hakuna aliyeendelea kupinga kimahakama, suala hili lichukuliwe kwamba limefikia mwisho na limefungwa. Lakini hata kiuongozi, na hasa kwa mtu yeyote mwenye kutazama maslahi ya Taifa hili, ni dhahiri kwamba suala la utekelezaji wa mikataba ya kubadilishana madeni ni jambo lenye manufaa kwa Tanzania na linapaswa kila fursa inapojitokeza kutekelezwa haraka.
Wenzetu, nchi wafadhili, wanapotoa fursa za kutupunguzia mzigo wa madeni katika utaratibu wenye manufaa kama huu, tutaendelea kuonekana wa ajabu kama tutaendelea kulumbana badala ya kuchangamkia fursa ya maendeleo. Tukwepe mazingira yanayopelekea taifa letu kuonekana kama wale watoto watukutu waliokabidhiwa zawadi ya nyumba, badala ya kuishi kwa shukrani ya nyumba ile, wakagombana na kunyang’anyana fito na kuzitumia kupigana bila kujali kwamba nyumba inaanguka maana fito ndizo zilizo ishikilia.
16.0 Mimi kama Mbunge kutokea Mkoa wa Lindi, na kama Waziri mwenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, nalifuatilia kwa karibu suala hili kwa sababu mbili:-
(i) Kwanza, kuanzishwa kwa mradi huu kutawanufaisha wapiga kura wangu, na Watanzania kwa ujumla kwa kuinua uchumi wetu na kuongeza ajira hasa wa Mikoa ya Kusini ambayo imeachwa nyuma kwa muda mrefu. Utafiti unaonyesha kuwa Mikoa ya Lindi na Mtwara ina utajiri mkubwa wa mali ghafi ya Saruji, na kwa hiyo upo uhakika wa kupata saruji bora na kwa bei nafuu sana.
(ii) Pili, suala hili linagusa mahusiano ya Nchi mbili kwa hiyo lazima Wizara yangu ilisimamie kwa nguvu, umahiri na umakini wote.
17.0 Kama nilivyosema huko nyuma, fedha zote zilizotolewa kwa amri ya Mahakama ni Mkopo. Hazikuchukuliwa kama fedha za EPA au ESCROW. Ni mkopo uliotolewa kwa Kampuni ya MEIS kwa mujibu wa Mkataba wa Makubaliano (Investment Agreement) yenye Masharti Kibenki. Na Masharti hayo ya Kibenki yanamtaka Mwekezaji kuweka dhamana, kulipia riba, kuwekewa muda wa kurudisha mkopo, na anawekewa hatua za kuchukuliwa endapo Mwekezaji huyo atashindwa kulipa mkopo. Kwa lugha nyingine, Kampuni ya MEIS ikishindwa kulipa mkopo huo, itafilisiwa mali zake na TIB itarudishiwa fedha zake. Iacheni benki ifanye kazi yake. Mkopo unageukaje kuwa ufisadi?
18.0 Mimi sina Kampuni hapa nchini. Sina ubia na kampuni yoyote ikiwemo Kampuni ya MEIS. Sina hisa katika Kampuni ya MEIS. Na sijafaidika na mkopo huo ambao unasimamiwa na Benki ya Uwekezaji nchini (TIB). Ndiyo maana uvumi kuwa nahusika na ufisadi wa mabilioni ya Libya hauna mashiko kabisa. Baadhi ya wanasiasa wenzangu wanajua ukweli wote huu lakini kwa makusudi wanaamua kuwafanya watu waamini wapinzani!
19.0 Ujenzi wa kiwanda cha simenti cha Lindi unaendelea vizuri na mitambo yote inayotakiwa katika ujenzi huo imekwisha wasili. Asilimia 45 ya ujenzi wa kiwanda hicho umekamilika na ni mategemeo ya kampuni ya MEIS kuwa kiwanda hicho kitakamilika ifikapo mwezi Disemba mwaka huu wa 2015.
20.0 Ni matumaini yangu kuwa nimeeleweka vya kutosha. Kama kuna mtu anahitaji taarifa zaidi basi awe huru kuihoji kampuni ya MEIS na Benki ya TIB ambayo imetoa mkopo huo, au kumpata Msajili wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa ambazo zote ziliamua Kampuni ya MEIS ipewe mkopo huo kwa mujibu wa sheria za kibenki.
Bernard K. Membe (Mb)
WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA
USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
2.0. Katika utaratibu huo wa ‘Dept Swap’, tarehe 20/7/2005, Serikali ya Tanzania na Libya zilitia sahihi mkataba wa Dept Swap (Dept Swap Agreement) ambao uliweka utaratibu wa matumizi na urejeshaji wa fedha za deni la Libya.
3.0. Tarehe 4/3/2009, Serikali ya Libya na Tanzania zilitia sahihi mkataba wa nyongeza (Addendum to the Dept Swap Agreement) ambao ulizungumzia, pamoja na mambo mengine, matumizi ya jumla ya dola za Kimarekani milioni 20 (20,000,000) ambazo zilikuwa zimehifadhiwa katika akaunti ya Libya No.004-200-0002216-01, Benki ya Rasilimali Tanzania (Tanzania Investment Bank).
4.0. Nyongeza hii ya mkataba ilitamka bayana katika kifungu No.4.02, kwamba, fedha zilizokuwa katika akaunti tajwa, zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua wao wenyewe, ambaye ni kampuni ya MEIS INDUSTRIES LIMITED kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha Saruji Lindi. Kwa mujibu wa nyongeza hii, mkopo ulipaswa kulipwa ndani ya miaka sita, na baada ya hapo, fedha hizo zirejeshwe na ziendelee kukopeshwa Watanzania kwa ajili ya miradi mingine ambayo Serikali za Libya na Tanzania zitakuwa zimeridhia.
5.0. Kumbukumbu zinaonyesha mambo mawili:-
5.1 Kwamba, kabla ya Serikali ya Libya kutia sahihi nyongeza hii ya mkataba iliyotaka fedha zikopeshwe kwa MEIS INDUSTRIES, upembuzi yakinifu wa mradi husika ulifanywa na serikali ya Libya kupitia vyombo vyake, na wao wenyewe walishajiridhisha juu ya ubora wa mradi huo (Viability of the Project)
5.2 Kwamba, baada ya kutia sahihi nyongeza ya mkataba, Serikali ya Libya kupitia Ubalozi wake hapa nchini iliendelea kusisitiza kwa maandishi kwamba Serikali ya Tanzania iharakishe mchakato wa kuwezesha fedha hizo zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua ili mradi huo muhimu usiendelee kuchelewa, na pia fedha ziingie katika mzunguko kwa manufaa ya Watanzania.
6.0. Katika kutekeleza mikataba hii miiwli, yaani Dept Swap Agreement ya tarehe 20/7/2005 na Addendum Dept Swap Agreement ya Tarehe 4/3/2009, na kwa kuzingatia umuhimu ambao serikali ya Libya iliuonyesha, Serikali ya Tanzania kupitia watalaamu wake wa Wizara ya Fedha, Benki ya Rasilimali (TIB) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, na Mwekezaji (Kampuni ya MEIS), walikutana chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na kuandaa hadidu za rejea ambazo zilipelekea kutengenezwa kwa mkataba wa uwekezaji (Investment Agreement) kati ya serikali ya Tanzania, TIB, Serikali ya Libya na Mwekezaji.
7.0. Serikali ya Tanzania, TIB na Mwekezaji walitia sahihi mkataba huu na kuupeleka Libya ili serikali ya Libya ipate kuweka sahihi. Kwa sababu ambazo hazikufahamika, serikali ya Libya haikutia sahihi mkataba huo.
8.0. Baada ya kufuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio, mwekezaji alimuandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania yenye kumbukumbu No. PC/MEIS/AG/2/10 ya tarehe 1/9/2010 akieleza kusudio la kuipeleka Serikali ya Libya Mahakamani kwa kitendo chake cha kutokutia sahihi mkataba.
9.0. Terehe 13/9/2010, Mwekezaji alifungua shauri Mahakama Kuu ya Tanzania, shauri la madai No. 124/2010 dhidi ya serikali ya Libya, akiiomba Mahakama Kuu itoe tamko kwamba kitendo cha serikali ya Libya kukataa kutia sahihi mkataba huu hakikuwa kitendo cha haki na kwamba mahakama itoe amri kwamba fedha hizo zitolewe kwa Mwekezaji ili kutekeleza mradi uliokusudiwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kwamba wito wa Mahakama (Summons) ulipelekwa Ubalozi wa Libya lakini hapakuwa na majibu wala mwakilishi aliyekuja mahakamani.
10.0. Mahakama Kuu, kwa kufuata taratibu zake, iliendelea na kusikiliza shauri na kutoa amri kama ambavyo mahakama yenyewe ilijiridhisha. Amri ya mahakama, pamoja na mambo mengine, iliagiza kwamba fedha hizo zitolewe kwa mwekezaji ili kutekeleza mradi husika.
11.0. Zilifanyika juhudi za Benki ya Rasilimali (TIB) pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupinga au kupata ufafanuzi zaidi juu ya amri hiyo ya utekelezaji wake. Mahakama Kuu pamoja na Mahakama ya Rufana, katika nyakati tofauti, zilishughulikia maombi hayo na kuyafikisha katika hatima yake kwa mujibu wa sheria. Kwa ajili ya kumbukumbu, mashauri yaliyofunguliwa ni kama ifuatavyo:-
11.1 TIB ilifungua maombi No. 126/2010 katika mahakama ya Rufaa kuiomba izuie na kufuta utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu. Maombi haya ya TIB yalifanyiwa uamuzi wa mwisho mnamo tarehe 7/11/2011, ambapo maombi hayo yaliondolewa mahakamani kwa kuwa, kwa mujibu wa Mahakama ya Rufaa, hayakuwa yamefuata taratibu za kisheria.
11.2 Mwanasheria Mkuu wa Serikali naye akapeleka maombi Mahakama ya Rufaa. Maombi ya kwanza, maombi namba .146/2010 akiomba Mahakama ya Rufaa kufuta mwenendo mzima wa kesi pamoja na amri ya Mahakama Kuu, na maombi ya pili No. 147/2010 ikiiomba Mahakama ya Rufaa izuie utekelezaji wa amri ya mahakama Kuu (Stay of Execution). Maombi haya yote yalisikilizwa na kuamuliwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za kimahakama.
12.0 Wakati haya yakiendelea, ilijitokeza kampuni ya Mohamed Enterprises Limited ikidai kwamba ina haki juu ya fedha hizi. Nayo ikafanya yafuatayo:-
12.1 Ilipelea maombi Mahakama Kuu kuzuia utekelezaji wa hukumu kwa madai kuwa kampuni hiyo nayo ilikuwa ikiishtaki Serikali ya Libya katika kesi ya madai No. 110/2010 na kwa hiyo, endapo amri ya Mahakama Kuu ingetekelezwa kwa kumpa mwekezaji (Kampuni ya MEIS) fedha za Libya, basi wao (Mohamed Enterprises Limited) wangekosa mahali pa kutekeleza/kukazia hukumu waliyokuwa wakiitarajia katika kesi yao (no. 110/2010) dhidi ya serikali ya Libya. Maombi haya yalisikilizwa na Mahakama Kuu na kutolewa maamuzi stahiki.
12.2. Kampuni ya Mohamed Enterprises Limited haikuridhika na uamuzi wa Mahakama Kuu kwa hiyo kapeleka shauri hili Mahakama ya Rufaa, kupitia maombi (Civil Revision) No. 2/2011. Maombi haya nayo pia yalisikilizwa na kutolewa maamuzi.
13 Mwisho wa yote maamuzi ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa katika mchakato mzima yakawa kwamba mwekezaji (Kampuni ya MEIS) alikuwa na haki ya kupewa fedha za mradi wa Kiwanda cha Saruji Lindi kama ilivyoanishwa katika mkataba kati ya serikali ya Tanzania na Libya. Ni dhahiri kwamba, mgogoro huu ulichujwa na mahakama mpaka ngazi ya juu kabisa, tena kwa nyakati tofauti na mbele ya waheshimiwa majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.
14.0 Katika Taifa linaloongozwa kikatiba, chini ya utawala wa sheria kama Tanzania, ambapo Mahakama ndicho chombo kilichopewa mamlaka ya mwisho kuamua juu ya haki za raia na hata serikali, si rahisi na wala haitakuwa sahihi kwa mtu yeyote kuhoji uhalali wa mchakato huu kama ulivyoongozwa, kuelekezwa na kuamuliwa na mahakama, isipokuwa tu kama sheria inatoa mwanya mwingine kurudi mahakamani kwa mtu yeyote ambaye hajaridhika au anayetaka kuhoji maamuzi haya kwa namna yoyote.
15. Mahakama iliamua kwa mujibu wa sheria. Na kwa kuwa hakuna aliyeendelea kupinga kimahakama, suala hili lichukuliwe kwamba limefikia mwisho na limefungwa. Lakini hata kiuongozi, na hasa kwa mtu yeyote mwenye kutazama maslahi ya Taifa hili, ni dhahiri kwamba suala la utekelezaji wa mikataba ya kubadilishana madeni ni jambo lenye manufaa kwa Tanzania na linapaswa kila fursa inapojitokeza kutekelezwa haraka.
Wenzetu, nchi wafadhili, wanapotoa fursa za kutupunguzia mzigo wa madeni katika utaratibu wenye manufaa kama huu, tutaendelea kuonekana wa ajabu kama tutaendelea kulumbana badala ya kuchangamkia fursa ya maendeleo. Tukwepe mazingira yanayopelekea taifa letu kuonekana kama wale watoto watukutu waliokabidhiwa zawadi ya nyumba, badala ya kuishi kwa shukrani ya nyumba ile, wakagombana na kunyang’anyana fito na kuzitumia kupigana bila kujali kwamba nyumba inaanguka maana fito ndizo zilizo ishikilia.
16.0 Mimi kama Mbunge kutokea Mkoa wa Lindi, na kama Waziri mwenye dhamana ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, nalifuatilia kwa karibu suala hili kwa sababu mbili:-
(i) Kwanza, kuanzishwa kwa mradi huu kutawanufaisha wapiga kura wangu, na Watanzania kwa ujumla kwa kuinua uchumi wetu na kuongeza ajira hasa wa Mikoa ya Kusini ambayo imeachwa nyuma kwa muda mrefu. Utafiti unaonyesha kuwa Mikoa ya Lindi na Mtwara ina utajiri mkubwa wa mali ghafi ya Saruji, na kwa hiyo upo uhakika wa kupata saruji bora na kwa bei nafuu sana.
(ii) Pili, suala hili linagusa mahusiano ya Nchi mbili kwa hiyo lazima Wizara yangu ilisimamie kwa nguvu, umahiri na umakini wote.
17.0 Kama nilivyosema huko nyuma, fedha zote zilizotolewa kwa amri ya Mahakama ni Mkopo. Hazikuchukuliwa kama fedha za EPA au ESCROW. Ni mkopo uliotolewa kwa Kampuni ya MEIS kwa mujibu wa Mkataba wa Makubaliano (Investment Agreement) yenye Masharti Kibenki. Na Masharti hayo ya Kibenki yanamtaka Mwekezaji kuweka dhamana, kulipia riba, kuwekewa muda wa kurudisha mkopo, na anawekewa hatua za kuchukuliwa endapo Mwekezaji huyo atashindwa kulipa mkopo. Kwa lugha nyingine, Kampuni ya MEIS ikishindwa kulipa mkopo huo, itafilisiwa mali zake na TIB itarudishiwa fedha zake. Iacheni benki ifanye kazi yake. Mkopo unageukaje kuwa ufisadi?
18.0 Mimi sina Kampuni hapa nchini. Sina ubia na kampuni yoyote ikiwemo Kampuni ya MEIS. Sina hisa katika Kampuni ya MEIS. Na sijafaidika na mkopo huo ambao unasimamiwa na Benki ya Uwekezaji nchini (TIB). Ndiyo maana uvumi kuwa nahusika na ufisadi wa mabilioni ya Libya hauna mashiko kabisa. Baadhi ya wanasiasa wenzangu wanajua ukweli wote huu lakini kwa makusudi wanaamua kuwafanya watu waamini wapinzani!
19.0 Ujenzi wa kiwanda cha simenti cha Lindi unaendelea vizuri na mitambo yote inayotakiwa katika ujenzi huo imekwisha wasili. Asilimia 45 ya ujenzi wa kiwanda hicho umekamilika na ni mategemeo ya kampuni ya MEIS kuwa kiwanda hicho kitakamilika ifikapo mwezi Disemba mwaka huu wa 2015.
20.0 Ni matumaini yangu kuwa nimeeleweka vya kutosha. Kama kuna mtu anahitaji taarifa zaidi basi awe huru kuihoji kampuni ya MEIS na Benki ya TIB ambayo imetoa mkopo huo, au kumpata Msajili wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa ambazo zote ziliamua Kampuni ya MEIS ipewe mkopo huo kwa mujibu wa sheria za kibenki.
Bernard K. Membe (Mb)
WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA
USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Monday, 29 June 2015
Said Ntimizi akamatwa kwa mauaji
Mtoto wa Waziri wa Zamani, Tatu Ntimizi anaeitwa Said Ntimizi ametiwa mbaroni kwa tuhuma za mauwaji.
Afya Maambukizo katika njia ya Mkojo (UTI)
Ni matumaini yangu kuwa hamjambo wapenzi
wasikilizaji na karibuni katika kipindi chenu chenye faida tele cha
Ijue Afya Yako. Leo tutazungumzia tatizo la maambukizi katika njia ya
mkojo Urinary Tract Infection ugonjwa ambao unawasumbua sana wanawake
wengi na watoto katika nchi nyingi zinzoendelea.
&&&&&&
Maambukizi katika njia ya mkojo au kama unavyojulikana kwa wengi UTI huathiri mfumo wa mkojo ikiwa ni pamoja na ureter ambayo ni kama bomba linalosafirisha mkojo kutoka kwenye figo, pia kibofu cha mkojo na urethra. Ugonjwa huu unaathiri zaidi kibofu cha mkojo na urethra lakini unaweza pia kuathiri figo. Maambukizi haya yakiathiri sehemu za chini za kibofu cha mkojo kitaalamu huitwa simple cystitis au Bladder infection, na maambukizi hayo yakitokea sehemu za juu za mfumo wa mkojo huitwa pylonephritis au kidney infection. Ugonjwa huu husababishwa na bakteria anayeitwa Escherichia coli (E. coli) na tatizo hili husababishwa kwa kiasi kikubwa na bakteria ambao makazi yao ya kawaida ni kwenye utumbo mpana, na hivyo huwa wanapatikana pia kwenye haja kubwa. Lakini baadhi ya watu wanaweza kupata tatizo hili kutokana na kuingiwa na fangasi ingawa pia zipo sababu nyingine chache. Bakteria wa Escherichia coli hawasababishi peke yao UTI bali huambatana na wengine waitwao staphylococcus, saprophyti cus, pseudom onas, enterobacter na kadhalika. Maambukizi katika njia ya mkojo lazima yawe ni kwenye njia ya mkojo na si pengine popote. Wapo wanawake ambao wamekuwa wakidhani kwamba tatizo la kutokwa na uchafu ukeni ni ugonjwa huu, na hilo si sawa kwani huo ni ugonjwa tofauti kabisa na UTI. Tunapozungumzia maambukizi katika njia ya mkojo, inamaanisha ni kutoka eneo la nje ya utupu hadi kwenye kibofu na kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo. Kama maambukizi yako katika eneo la kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo, kitaalamu huitwa Lower Urinary Tract Infection na yakihusisha eneo la juu ya kibofu jina hubadilika na kuitwa, Upper Urinary Tract Infection. Mara nyingi maambukizi haya kwa wanawake husababishwa na kutojisafisha vizuri sehemu za siri na kuvaa nguo za ndani zilizochafu. Pia huweza kusababishwa na matumizi ya pedi za kike zenye kemikali ya kukata harufu ambazo huua bakteria wa asili wa eneo la uke na kuwapa fursa bakteria wanaosababisha maradhi kuzaliana kwa wingi. Halikadhalika upungufu wa homoni ya wanawake iitwayo Oestrogen husababisha bakteria wanaosababisha maambukizi katika njia ya mkojo kuzaliana kirahisi. Matumizi ya baadhi ya dawa kwa muda mrefu, unywaji wa vinywaji vyenye sukari kwa muda mrefu na kutokunywa maji ya kutosha pia huchangia tatizo hili. Uwepo wa mawe katika figo na mirija ya figo pia ni mojawapo ya chanzo cha maambukizi haya katika njia ya mkojo. Sababu nyingine inayosababisha UTI ni matumizi ya maji machafu wakati wa kujisafisha au kuoga ambayo huweza kuweka bakteria kwa urahisi na kupelekea mwanamke kupata ugonjwa huo. Uchafu wa vyoo umetajwa kuwa sababu nyingine, kwani matumizi ya vyoo ambavyo ni vichafu huweza kusababisha mwanamke kupata UTI kwa sababu ndani ya choo kuna bakteria wengi ambao wanaweza kusababisha ugonjwa huo.
&&&&&&
Matatizo haya ya maambukizi licha ya kuwapata zaidi wanawake, huwakumba pia watoto wadogo wa kike kutokana na sababu za kimaumbile ambapo viungo vyao vya uzazi, njia ya mkojo na haja kubwa vipo jirani. Watoto wa kiume ambao hawajatahiriwa nao huweza kupata maambukizi rahisi ya UTI iwapo watajisafisha kwa kutumia maji yasiyo salama ambapo huwa rahisi kwa bakteria kubaki katika ngozi inayoning'inia (govi). Pia wanaume watu wazima ambao hawajatahiriwa wanaweza kupata maambuzi ya UTI kutokana na sababu tuliyoitaja ambapo pia ni rahisi kwao kuambukizwa Ukimwi kama watafanya ngono zembe na ndiyo maana tohara kwa wanaume husisitizwa.
Maambukizi yanayoshambulia mfumo wa mkojo husababishwa zaidi na bakteria wanaoishi katika mfumo wa haja kubwa kwa kuingia na kujikita katika mfumo wa mkojo. Bakteria wengine wanaoleta maabukizo katika njia ya mkojo ni wale watokanao na magonjwa ya zinaa kama kisonono, klamidia, trimonas na fangasi ambapo huwaathiri watu pale wanapojamiiana bila kutumia kinga na watu wenye maradhi hayo. Ili kuepuka kupata maambukizi katika njia ya mkojo, mara kwa mara, ni vyema kutumia kinga na kwa mwanamke wanashauri kila wanapomaliza kufanya tendo la ndoa wakojoe ili kuondoa bakteria walioingia au waliokaa katika tundu ya mkojo wakisubiri kuingia. Baada ya kujua hayo yote hivi sasa tuzijadili dalili za ugonjwa wa UTI.
Baadhi ya dalili za mtu kuambukizwa bakteria katika njia ya mkojo kubwa ni maumivu wakati wa kukojoa, mkojo kuwa na rangi ya njano kupindukia na kuwa na harufu kali ijapokuwa siyo kila mwenye dalili hizo ana maambukizi katika njia ya mkojo. Dalili nyingine za UTI ni maumivu, kutokwa na usaha wakati wa kukojoa, kabla au baada ya kukojoa kukiambatana na maumivu na kuhisi moto wakati mkojo ukitoka. Baadhi ya wanaume wakati mwingine hutokwa na majimaji katika njia ya mkojo wakati wa kujisaidia haja kubwa. Wengine wenye maambukizi hujikuta wakipata vichomi katika njia ya mkojo, au kuhisi kuwashwa sehemu hiyo, kuumwa kiuno au tumbo na kadhalika. Mgonjwa anaweza pia kukumbwa na homa kali mara kwa mara na mwili kuwa mchovu, kwa watoto hupoteza hamu ya kula na mwili huonesha kuchoka.
Wagonjwa wengine hupata maumivu kwenye kibofu cha mkojo ambapo husikia maumivu ya chini ya tumbo usawa wa kitovu na huwa hayaishi. Matatizo haya ya mfumo wa mkojo kama tulivyoona kabla huwapata watu wote wanawake na wanaume. Watu wenye matatizo haya kila wakipima huambiwa wana UTI. Kwa wanaume huhisi hata nguvu za kiume kupungua na wanawake hupoteza hamu ya tendo la ndoa.
Kwa wajawazito ugonjwa unaweza kuhatarisha maisha yao na mtoto aliye tumboni. Bakteria wanaweza kuingilia mfumo wa damu na kusababisha madhara mengine kama vile shinikizo la damu kuwa kubwa kwenye figo na hata kusababisha ufanyaji kazi mbovu wa figo.
&&&&&
Maambukizi katika njia ya mkojo hutibika kwa dawa mbalimbali za kisasa baada ya kufanyiwa vipimo na kuthibitika kuwa mgonjwa ana maambukizi hayo. Dawa ambazo anaweza kupewa ni kama vile Ciprofloxacin, Monurol, Furadantin, Sulfam ethoxazole, co-trimax, ampicillin, gentamicin na kadhalika. Mgonjwa anayesumbuliwa na UTI hapaswi kutumia dawa yoyote bila kwanza kupata ushauri wa daktari.
Wanawake wanashauriwa kuepuka kujisafisha sehemu za siri na maji machafu na yasiyo salama, pia kuepeuka kupaka marashi sehemu hizo, ama kutumia pamba zenye kemikali ya kukata harufu kwani hizo huua bakteria wa asili wa ukeni hali ambayo hukaribisha bakteria wa maradhi kuzaliana kwa wingi. Pia wanashauriwa wanapojisafisha baada ya kujisaidia kuanzia mbele kwenda nyuma, ili kuepusha kuhamisha bakteria walio eneo la haja kubwa na kuingia njia ya mkojo. Kwa wale walio katika kipindi cha ukomo wa hedhi, wanaweza kushauriana na daktari juu ya kutumia oestrogen ya ukeni ili kuwasaidia kujikinga na maambukizi ya UTI. Kwa mwanaume maambukizi haya huathiri nguvu za kiume na kujipenyeza hadi katika korodani na huathiri uzalishaji wa mbegu za kiume na kunaweza hata kusababisha mgumba. Hivyo wanashauriwa kuhakikisha wanatibu bila kuchelewa ugonjw ahuo. Pia maambukizi ya njia ya mkojo huweza kusababisha matatizo ya tezi ya kiume (prostate) kwani husababisha mrija wa mkojo kuziba, kutopitisha mkojo vizuri na kuruhusu bakteria kujenga makazi. Hali hiyo ikitokea mgonjwa lazima akamuone daktari ili awekewe mrija wa kutolea mkojo.
Mpenzi msikilizaji madaktari wanatueleza kuwa, tunaweza kuudhibiti au kuponya ugonjwa huu kwa kunywa maji mengi pamoja na juisi itokanayo na matunda halisi, iwapo tutawahi kabla tatizo halijawa sugu. Kwa maana nyingine, unaweza kujikinga na ugonjwa huu kwa kuwa na mazoea ya kunywa maji ya kutosha kila siku. Ukinywa maji ya kutosha yatakufanya uende haja ndogo kila mara na kwa njia hiyo wale bakteria watakuwa wakitoka na hatimaye kuisha kabisa. Katika hali ya kawaida, ugonjwa wa UTI hutoweka ndani ya siku tatu mara baada ya kuanza kutumia tiba asili ya kunywa maji mengi na juisi ya matunda halisi, iwapo ugonjwa utaendelea kuwepo baada ya siku hizo, hiyo itakuwa na maana ugonjwa wako umeshakomaa na hivyo hauwezi kutibika kwa tiba hii ya nyumbani na itakuwa inapaswa kwenda hospitalini na kuonana na daktari ambaye atafanya uchunguzi na kutoa dozi sahihi ya kutibu ugonjwa huo.
Wasikilizaji wapenzi tutaendelea kujadili ugonjwa wa maambukizo katika njia ya mkojo kwenye kipindi chetu kijacho. Hadi wakati huo tusisahau kuzilinda afya zetu na kwaherini.
CHANZO: IRAN SWAHILI REDIO
Subscribe to:
Posts (Atom)





