Monday, 13 July 2015

Mzungu mchochezi anaswa Loliondo


Sweden, Susanna Nordlund, anayetambuliwa kama mmoja wa wachochezi wakuu wa migogoro katika eneo la Loliondo, Ngorongoro mkoani Arusha, amekamatwa na kufukuzwa nchini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkuu wa Wilaya (DC) ya Ngorongoro, Hashim Shaibu, ndiye aliyeongoza Kamati hiyo kwenda kumkamata.
Sussana alikamatwa saa 2 usiku katika hoteli maarufu ya Onesmo iliyopo Wasso, akiwa anakula chakula.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa alifikia katika nyumba ya kulala wageni inayomilikiwa na aliyekuwa Mbunge wa Ngorongoro, ole Mathew Timan pamoja na mkewe, Tina.
Tina ni Mkenya aliyepata uraia wa Tanzania mwaka 2010. Ni Mbunge wa Viti Maalumu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwa amepata nafasi hiyo kabla ya kuwa raia wa Tanzania. Anatuhumiwa kuwa miongoni mwa wachochezi wakuu wa migogoro katika Loliondo na Ngorongoro kwa jumla.
Susanna amekuwa akijiamini mno, hasa kutokana na kile anachosema kwamba endapo Serikali itaendelea kumfuata fuata, atahakikisha Sweden inakata misaada yake nchini.

“Tumesema sisi si maskini kiasi cha mtu kuvuruga nchi yetu kwa kigezo kuwa atatucongea ili tusipate misaada kutoka kwao. Ina maana tunapewa misaada kwa kigezo cha kutuvuruga?” Amesema mmoja wa viongozi walioshiriki kumkamata.
Hii si mara ya kwanza kwa Susanna kuingia nchini licha ya kuwa na PI. Kwenye mtandao wake wa Just Conservation, anatamba na kuonyesha namna alivyoweza kurejea nchini, kuzunguka na kufanya kilichomleta bila kuguswa. Hiyo ilikuwa Julai, 2013.
Shaibu amezungumza na JAMHURI na kuthibitisha kukamatwa kwa Mswiden huyo na kusema familia ya Timan inahojiwa kwa kumhifadhi Susanna.

Shaibu amesema mahojiano hayo yanalenga hasa kujua sababu za kumhifadhi Susanna ambaye kina Timan wanatambua kuwa alishapewa hati ya kufukuzwa nchini (PI) tangu mwakja 2010.
“Tulimkamata Juni 23 usiku. Alipohojiwa alikutwa na viti vingi ambavyo vingine ni hatari kwa usalama wa nchi. Alikuwa na questionnaire (maswali) mengi sana aliyopanga kuwauliza wanavijiji wa Oloipir, Mondorosi, Sukenya na vingine. Ni maswali ya uchochezi kabisa,” amesema DC Shaibu.
Amesema kwenye upekuzi huo ilibainika aliingia nchini kupitia mpaka wa Namanga akiwa na hatia ya kusafiria ikimwonyesha kuwa ni mtalii.
“Tulikaa naye hapa Loliondo (rumande) kwa siku tatu tukaona ni busara kumpeleka katika ngazi za juu mkoani. Mimi kama DC niliishia hapo,” amesema.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Tibenda Kijiko, hakuweza kupatikana kuelezea hatima ya mchochezi huyo.

Hata hivyo,  Kamishna wa Huduma za Uhamiaji na Udhibiti wa Mipaka, Abdallah Abdullah, ameliambia JAMHURI kwamba Susanna baada ya kushikiliwa Loliondo na Arusha, alifukuzwa nchini.
Alipoulizwa imekuwaje mtu aliyepewa PI akaweza kurejea nchini bila kutambuliwa kwenye mifumo ya utambuzi ya kisasa, Kamishna Abdullah amesema: “Alipofukuzwa nchini mwaka 2010 mfumo wa utambuzi wa kutumia kompyuta ulikuwa bado. Ilibidi tufukue nyaraka kuweza kutambua kuwa alishafukuzwa.
“Hivi sasa baada ya kubaini hilo taarifa zote zinazomhusu tumeshaziingiza kwenye mtandao. Akiingia tu, akigusa dole gumba kwenye mashine mara moja atatambulika.”
Amesema wenyeji waliotumika kumhifadhi wanaendelea kuhojiwa na sheria za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“Hapa tumesema hatuna huruma kwa watu wanaoshirikiana na wageni kuihujumu nchi yetu. Wananchi waendelee kutupatia taarifa za wageni na watu wanaowahifadhi.
“Mtu anajua kabisa huyu mgeni hatakiwi nchini, badala ya kumzuia yeye anamkaribisha. Mbaya zaidi hata kwenye hoteli hakuandika jina lake kwenye kitabu cha wageni. Hii ni kuonyesha kwamba walijua kinachofanywa na huyo mgeni,” amesema.
Kamishna Abdullah amemwagia sifa DC Shaibu kwa kusema muda mfupi alioshika madaraka hayo, Ngorongoro imekuwa na mabadiliko makubwa kwenye Uhamiaji.
“Amefanya kazi kubwa na nzuri sana kwa muda mfupi. Kazi yake imetusaidia sana, ni msikivu na anaonekana ana dhamira ya kuifanya Ngorongoro iwe sehemu salama,” amesema Kamishna huyo.
Awali, Susanna alifanya mikutano ya siri katika maeneo ya Kertalo na Karkamoru akiwa na Tina.

Mmoja wa wananchi wanaokerwa na uchochezi unaofanywa na asasi zisizo za serikali (NGO) amesema: “Nadhani kwa upeo wangu hizi ni harakati za kijasusi za wazungu na ukoloni mamboleo kutikisa Serikali ya Tanzania (To destabilize Tanzania Government wakimtumia Susanna Nordlung, wafadhili wa mataifa ya Magharibi, na mashirika ya kimataifa.
Wanazijengea uwezo NGOs zote za Wamasaai wa Kenya na Tanzania ili baadaye waweze kurudisha ardhi za Wamasai zilizochukuliwa na wakoloni wa Kiingereza na baadaye serikali za Tanzania na Kenya.

“Ardhi hizi kwa upande wa Tanzania ni Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, na Pori Tengefu la Loliondo kama sehemu za kuanzia na baadaye Hifadhi za Mikumi, Tarangire, nk.
“Mikakati ni kuunganisha umoja na NGOs za Kimasai ili wote wa Tanzania na Kenya waungane. Hawa watu (wafadhili wa Magharibi) siyo wazuri sana. Sasa hivi chunguza mabilioni ya fedha ambazo mashirika haya inazo pamoja na blogs. Ni hatari.”
Kwa muda sasa, Susanna na wadau wenzake wamekuwa wakikusanya mabilioni ya fedha kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa kile anachosema ni kwa ajili ya kuwasaidia wafugaji na wenyeji “wanaonyanyaswa” katika maeneo yao.
Kupitia ufadhili wake, amekuwa akizimwagia NGOs fedha nyingi, huku silaha kuu ya kuhakikisha shughuli hiyo inaendelea ni kupandikiza migogoro ya mara kwa mara.
CREDIT: JAMHURI MEDIA

Wachina wabuni uhujumu uchumi mwingine


Kwa sasa kumetokea mchezo mchafu unaofanywa na raia wa China na Singapore walio hapa nchini. Mchezo huu umeshamiri baada ya baadhi ya Wachina wasio waaminifu kushiriki biashara ya pembe za ndovu.
Wameanzisha utaratibu wa kusajili kampuni za kusafirisha samaki hai aina ya kaa na kamba kochi kwenda nje kwa kutumia kampuni zenye majina ya wazawa.
Wanachofanya ni kutafuta Mtanzania, wanampa pesa anakwenda idara zote zinazohusika na biashara hii. Wanasajili kampuni kwa kutumia majina ya Watanzania. Akishamaliza taratibu zote anakabidhiwa raia wa nje kinyume cha sheria ya Wizara ya Maendeleo Mifugo na Uvuvi, inayosema leseni haitakiwi kuazimishwa kwa mtu yeyote; na raia wa kigeni hawatakiwi kufanya hii biashara.

Wanatumia mawakala kuwanunulia kaa na kamba kochi hai, maana wao hawataki waonekane kwa sababu wanavunja sheria za nchi. Hata kwenda uwanja wa ndege watumia mawakala.
Mazao ya baharini yaliyovamiwa sana ni kamba kochi hai na kaa hai maana ndiyo yenye soko kubwa kwao. Nchi zinazoongoza kwa kununua kaa na kamba kochi hai wadogo sana na wenye mayai ni China na Hong Kong. Kwa wanavyonunua kwa wingi tusitarajie baada ya miaka miwili kutakuwa na viumbe hivyo hapa nchini. Kampuni vinara wa kusafirisha mizigo ya Wachina ni KN Marine, Marine Food Products Ltd, Sasha Marine Enterprise na NF Trading Co. Zote zina majina ya Watanzania, lakini zinatumiwa na Wachina. Kinara mkuu wa hii biashara haramu ni (jina tunalihifadhi kwa sasa). Amejenga mtandao mkubwa kuanzia Idara ya Uvuvi hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Amesajili kampuni zaidi ya nne kwa kutumia majina ya jamaa zake na marafiki zake wazawa, lakini zote zinatumiwa na Wachina na Wasingapore. Kinara mwingine yupo (jina tunalihifadhi kwa sasa).

Wachina hawa wananunua kaa na kamba kochi hai, wanakaa nao makwao walikopanga na wengine watumia viwanda walivyosajili kimagendo. Siku ya kusafirisha mzigo wanafunga kwenye maboksi, wakimaliza kufunga na kuweka lebo kuonesha anayesafirisha na kupokea mzigo huko nje kuendana na kampuni zilizosajiliwa hapa nchini, wanamtaarifu wakala kwamba anazo kilo ngapi na maboksi mangapi.
Wakala anakwenda Idara ya Uvuvi kukata vibali vya huo mzigo, kisha dereva anapeleka uwanja wa ndege. Dereva akitoka uwanja wa ndege na wakala anapeleka karatasi alizosafirishia mzigo kwa Wachina wanalipana pesa za uwakala. Kazi anayobaki nayo Mchina ni kutuma karatasi za mzigo kwao kwa faksi au kwa barua pepe ili mzigo ukachukuliwe uwanja wa ndege unakofikia.

Wakati wa kufunga mzigo wanaokuwapo ni Wachina na baadhi ya wafanyakazi wa Wachina wenye uelewa mdogo. Kinachofungwa humo wanakijua wao chini ya maboksi. Wakala (mzawa mwenye kampuni) anapokea tu uwanja wa ndege. Na kwa kuwa wana mtandao mkubwa, uwanja wa ndege wanapitisha hata kama kuna kaa wadogo, majongoo bahari na vitu vingine ndani.
Bei zao na zenyewe zinatia shaka kama kweli wanafanya hii biashara pekee, au wanatakatisha pesa wanazopata kwenye biashara nyingine, maana wananunua bei kubwa mno hapa nchini kiasi kwamba ukitoa na gharama za kuendesha kampuni, huwezi kupata kitu chochote.
Baadhi ya maafisa wa uvuvi wanawajua, lakini kutokana na kukithiri kwa rushwa, hawachukui hatua kali kukomesha hii hali, au kutotoa leseni holela za kusafirisha mazao ya baharini.

Watanzania waliosajili hizi kampuni wanachopata ni pesa ndogo wanayokubaliana kwa mwezi, kwa mwaka au kila mzigo unaposafirishwa.
Wanasafirisha kaa na kamba hai – wakubwa hadi wadogo kuanzia gramu 150 ambao hawaruhusiwi kisheria – kaa ambao hawajaanza kuzaa. Hao raia wa kigeni hawana uchungu na haya mazao ya bahari kwa sababu wanajua yakiisha watakwenda nchi nyingine ambako yanapatikana.
Kisheria wanaoruhusiwa ni kuanzia gramu 500 na kuendelea ndiyo wasafirishwe au kuvuliwa baharini.
Wazawa waliokuwa wanafanya biashara hii kihalali wameshindwa kwa sababu wananunua kuanzia wadogo sana mpaka wakubwa, wavuvi wanawakimbilia Wachina kwa sababu wananunua kaa wao wote. Sababu ya pili, wametumwa na kampuni zao kuja kukusanya na kuuza kule kwao kwa bei ya rejareja, hivyo ni ngumu kwa wazawa kushindana nao maana hatuna kampuni kwao. Wanatoa bei ndogo kwetu ili kampuni zetu zife wabaki wao kwenye soko la kununua na kusafirisha.

Faida yote inabaki kwao. Kinachorudi hapa ni pesa ya kununulia mzigo na kuendesha ofisi. Wengine wanatumia pesa wanayopata kwenye biashara nyingine kama Kariakoo ndiyo wanayonunulia samaki na nchi inakosa mapato ya kigeni.
Wanachama wa Chama cha Kusafirisha na Kuagiza nje Samaki (DAFIE) yaani Dar es Salaam Association of Fish Importers and Exporters wameshalalamika sana kuhusu hiyo biashara haramu na kuwaonya wahusika, lakini haikomi. Idara ya Uvuvi inatoa ushirikiano mdogo.
Badala ya hawa wazawa kuacha kubeba Wachina, wengine sasa wana Wachina zaidi ya watatu wanatumia leseni moja maana wameshanogewa. Miaka ya nyuma walipobanwa kwenye mkutano, kuna baadhi walikiri hadharani kwamba wanafanya hivyo kwa sababu hawana mitaji. Lakini kwa kadiri siku zinavyozidi kwenda hata baada ya kupata mtaji wamenogewa na hii biashara haramu hawataki kuiacha. Wanawaumiza wazawa wanaofanya biashara halali.

Ushahidi uko wazi kabisa. Ukienda Mbagala, Kigamboni, Soko la Samaki Ferry hadi Mkuranga wanakopokea mzigo kutoka Kusini, madalali wa kaa na kamba kochi wote wanajua kampuni zipi zinatumiwa na Wachina na zipi za wazawa. Hao ndiyo wapimaji na walipaji wa mzigo. Ukienda uwanja wa ndege ukafungua maboksi ya kaa na kamba wanaopelekwa China na Hong Kong, lazima utakuta kaa wadogo na wenye mayai. Kila siku mizigo inapita hapo.
Hii biashara haramu inafanywa kwa siri. Ukienda Idara ya Uvuvi wanakwambia aliyepeleka maombi ya leseni ni Mtanzania na ametimiza vigezo vyote ndiyo maana amepewa. Hata ukiwaambia kampuni fulani inafanya hivi au vile, wanataka ushahidi usiokuwa na shaka. Wakati mwingine wanasema sisi hatutaki au tunaogopa ushindani.

Hatukatai ushindani ila tushindane kwa njia sahihi na biashara endelevu. Baadhi  ya maafisa wanajua ila hawataki kutoa ushirikiano.
Tuna ushahidi mwingi. Mamlaka za juu zikitaka ushahidi tupo tayari kuzisaidia. Tulilo na hakika nalo ni kwamba Idara ya Uvuvi kwa sababu ya rushwa iliyokithiri, haiwezi kutoa ushirikiano.
Mwandishi wa taarifa hii amejitambulisha kuwa ni Mtanzania mzalendo. Ameomba jina lake lihifadhiwe, lakini amesema yupo tayari kuisaidia Serikali. Mawasiliano yote yapitie kwa Mhariri wa Gazeti la JAMHURI.

Burundi: Government forces clash with gunmen near border with Rwanda


Government troops have clashed with opposition gunmen in northern Burundi as tensions boil over near the Rwandan border amid the central African nation's worst political crisis since end of its civil war in 2005.

Army spokesman Colonel Gaspard Baratuza told AFP of shooting and "a situation of insecurity" near Rugazi, 140km (85 miles) north of the Burundian capital Bujumbura.

"An armed group attacked an army position... We heard shooting and the explosions of heavy weapons," a local government source told the French agency.

There are hopes tensions may ease in Burundi with the government's agreement to postpone controversial presidential elections.

The current crisis erupted in Burundi after an announcement by the country's president Pierre Nkurunziza that he would stand for a third term, despite two-term limits set in the country's constitution.

Over 70 people have been killed in the two months of ensuing violence. Over 158,000 refugees have fled to neighbouring countries as the country has destabilised, according to the UN.

The Burundian government has said it will postpone presidential elections until a few days after 15 July, when they were initially scheduled. However, the postponement is not as long as the two week period the East African Community (EAC) need to make progress with mediations.

On 9 July senior United Nations officials warned that the situation prevailing in the Central African country was once again at risk of sliding into violence.

"Burundi is on the brink again [and] the grave danger the country faces should not be underestimated, given the increasing polarisation and the apparent choice of Burundian leaders to put personal interest before those of the country," UN Assistant-Secretary-General for Political Affairs Taye-Brook Zerihoun told the UN security council.

"An escalating pattern of politically motivated violence, coupled with this country's history of recurring bloodshed and atrocities, should alert us to the potential for serious crisis," UN High Commissioner for Human Rights Zeid Ra'ad Al Hussein added.

One of the figureheads of Burundi's opposition, General Leonard Ngendakumana, who was part of a failed coup to topple Nkurunziza in 19 May, has said his group was still working to oust the president and accused him of stoking ethnic divisions that were the faultlines of the country's 12-year civil war.

Burundi's ruling party, the CNDD-FDD, won a landslide victory in parliamentary elections held across the country two weeks ago. However, amid a widespread opposition boycott of the polls, the international community has rejected the result stating that the elections took place under duress.


Bill Gates says he has no use for money… He is doing ‘God’s work’


Having already given away $28bn, Bill Gates intends to eradicate polio, with the same drive he brought to Microsoft .


William Henry “Bill” Gates is a rich man. His estimated wealth, some 65  billion measured in US dollars, equals the annual GDP of Ecuador, and maybe a bit more than that of Croatia. By this rather crude criterion, the founder of Microsoft is worth two Kenyas, three Trinidads and a dozen or so Montenegros. Not bad for a university dropout.

Gates is also mortal, although some of his admirers may find that hard to believe, and as they say, there are no pockets in shrouds. So he is now engaged in the process of ridding himself of all that money in the hope of extending the lives of others less fortunate than himself.

“I’m certainly well taken care of in terms of food and clothes,” he says, redundantly. “Money has no utility to me beyond a certain point. Its utility is entirely in building an organisation and getting the resources out to the poorest in the world.”

That “certain point” is set a little higher than for the rest of us – Gates owns a lakeside estate in Washington State worth about $150 million (£94  million) and boasting a swimming pool equipped with an underwater music system – but one gets the point. Being rich, even on the cosmic scale attained by Bill Gates, is no guarantee of an enduring place in history. The projection of the personal computer into daily life should do the trick for him, but even at the age of 57 he is a restless man and wants something more. The “more” is the eradication of a disease that has blighted untold numbers of lives: polio.



Later this month, Gates will deliver the BBC’s Dimbleby Lecture, taking as his theme the value of the young human being. Every child, he will say, has the right to a healthy and productive life, and he will explain how technology and innovation can help towards the attainment of that still-distant goal. Gates has put his money where his mouth is. He and his wife Melinda have so far given away $28 billion via their charitable foundation, more than $8  billion of it to improve global health.
“My wife and I had a long dialogue about how we were going to take the wealth that we’re lucky enough to have and give it back in a way that’s most impactful to the world,” he says. “Both of us worked at Microsoft and saw that if you take innovation and smart people, the ability to measure

what’s working, that you can pull together some pretty dramatic things.
“We’re focused on the help of the poorest in the world, which really drives you into vaccination. You can actually take a disease and get rid of it altogether, like we are doing with polio.”This has been done only once before in humans, with the eradication of smallpox in the 1970s.“Polio’s pretty special

because once you get an eradication you no longer have to spend money on it; it’s just there as a gift for the rest of time.”
One can see why that appeals to Gates. He has always sought neat, definitive solutions to things, but as he knows from Microsoft, bugs are resilient things. The disease is still endemic in Nigeria, Pakistan and Afghanistan, and killing it off altogether has been likened to

squeezing jelly to death. There is another, sinister obstacle: the propagation by Islamist groups of the belief that polio vaccination is a front for covert sterilisation and other western evils. Health workers in Pakistan have paid with their lives for involvement in the programme.
“It’s not going to stop us succeeding,” says Gates. “It does force us to sit down with the Pakistan government to renew

their commitments, see what they’re going to do in security and make changes to protect the women who are doing God’s work and getting out to these children and delivering the vaccine.”
Gates does not usually speak in religious terms, and has traditionally danced around the issue of God. His wife, a Roman Catholic, is less defensive on that topic but ploughs her own furrow, encouraging contraception when necessary, in contradiction to teaching from Rome.“Melinda and I had been talking about this even

before we were married,” he says. “When I was in my 40s Microsoft was my primary activity. The big switch for me was when I decided to make the foundation my primary purpose. It was a big change, although there are more in common with the two things than you might think – meeting with scientists, taking on tough challenges, people being sceptical that you can get things done.”
Gates is still chairman of Microsoft but without his day-to-day attention it has taken on the appearance of a weary giant,

trailing Apple and Google in innovation. Some have called for Gates’s return to the company full-time to inject some verve but he isn’t coming back.
“My full-time work for the rest of my life will be at the foundation,” he says. “I still work part-time for Microsoft. I’ve had two careers and I’m lucky that both of them have been quite amazing.“I loved my Microsoft: it prepared me for what I’m doing now. In the same way that I got to see the PC and internet revolutions, now I see child death rates coming down. I work very long hours and try to learn as much as I can about these things, but that’s because I enjoy it.”He emphasises that the

foundation’s effort is part of a global campaign in which governments must play the lead role.
“The scale of the (foundation’s) wealth compared to government budgets is actually not that large, and compared to the scale of some of these problems. But I do feel lucky that substantial resources are going back to make the world a more habitable place.”In 1990 some 12 million children under the age of five died. The figure today is about seven million, or 19,000 per day. According to the United Nations, the leading

causes of death are pneumonia (18 per cent), pre-birth complications (14 per cent), diarrhoea (11 per cent), complications during birth (nine per cent) and malaria (seven per cent). For Gates, though, polio is a totem. The abolition of the disease will be a headline-grabber, spurring countries on to greater efforts. The Bill and Melinda Gates Foundation will spend $1.8 billion in the next six years to accomplish that goal, almost a third of the global effort.
“All you need is over 90 per cent of children to have the vaccine drop three times and the disease stops spreading. The number of cases eventually goes to zero. When we started, we had over

400,000 children a year being paralysed and we are now down to under 1,000 cases a year. The great thing about finishing polio is that we’ll have resources to get going on malaria and measles.”
Gates is no saint. He could be an intimidating boss at Microsoft and his company became notorious for using its clout to reinforce its dominance in the market place, at the expense of smaller rivals.

Still, he and his wife are showing generosity on a staggering scale, a counterblast to the endemic greed of the Nineties and early Noughties, and they have convinced others that mega-philanthropy is the way of the future. That wily investor, Warren Buffett, has so far given away $17.5 billion via the Gates Foundation.
The children of Bill and Melinda Gates will never know poverty. They may not become multibillionaires but even the loss to charity of the vast bulk of their parents’ fortune should leave them with a billion or so each.Gates explains: “The vast majority of the wealth, over 95 per cent, goes to the foundation, which will spend all that money

within 20 years after neither of us are around any more.”
So, is it about some new-found faith, all this giving?“It doesn’t relate to any particular religion; it’s about human dignity and equality,” he says. “The golden rule that all lives have equal value and we should treat people as we would like to be treated.”

Source:
telegraph.co.uk

Sunday, 12 July 2015

Zitto amemtuma ofisa wake kuisemea CHADEMA kuhusu Lowassa!


Ofisa mmoja wa chama kiitwacho ACT ambaye mara kadhaa amenukuliwa akiwa ni msemaji wa chama hicho ameandika na kueneza habari mtandaoni kuwa kada mwandamizi wa CCM Edward Lowassa anahamia CHADEMA!

Inashangaza kidogo! Ama ni kwamba wahusika wa chama hicho hawana uratibu wa mawasiliano kiasi kwamba kila mtu anaweza kujiandikia tu au wanaendelea kukubuhu katika siasa nyepesi.

Itakumbukwa juzi mara baada tu ya majina 5 ya makada wa CCM yaliyokuwa yamepitishwa kwenye CC ya chama hicho kuwa yamejulikana (kwa kadri ya utaratibu wao) Kiongozi Mkuu wa ACT Zitto haraka haraka kama ilivyo kawaida yake akakimbilia mtandaoni kuandika kuwa Edward Lowassa anajiunga na ACT na atakabidhiwa kadi.

Wafuasi wa Zitto kwa kuendekeza siasa nyepesi za umaarufu wa mtu, wakakimbilia nao mitandaoni kusema kuwa tayari Lowassa ameshajiunga na ACT na kwamba ni Mgombea urais na 'taswira na nuru' ya chama tayari kapewa cheo cha Uwaziri Mkuu, alas!

Hawakuishia hapo. Wakaenda mbali hata kughushi nembo ya moja ya mashirika makubwa ya habari duniani kisha wakaandika mambo yanayokidhi matamanio yao, kwamba Lowassa kahamia ACT na Zitto kamkabidhi kadi.

Sasa haijajulikana hiyo kauli ya Zitto imeishia wapi ndani ya masaa 48 tu ghafla ofisa wake amekwenda mitandaoni akijigeuza kuwa msemaji wa taasisi isiyomhusu kuwa Lowassa amehamia CHADEMA.

Tumsaidie Zitto asiendelee kufanya siasa nyepesi. Alikuwa mtu wa kwanza kumkaribisha Lowassa kwenye chama chake mapema kabla hata hajachukua fomu ndani ya CCM. Sasa awaambie watu wake vizuri hilo 'deal' limeishia wapi?

Taarifa kutoka vyanzo vyangu zinasema kuwa Lowassa atafanya mkutano na waandishi wa habari kesho saa 3 huko Dodoma. Atakachozungumza anakijua vizuri yeye labda na watu wake pia.

Habari hizo kwamba Lowassa amehamia CHADEMA hazina ukweli wowote. Zinatengezwa na kupikwa na hao 'vijana' kwa maslahi wanayoyajua wao.

Kwa kushirikiana na vyama washirika wenza katika UKAWA, tunaendelea na maandalizi ya kwenda kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu, kushika dola na kuongoza serikali kuwatumikia Watanzania. Kila kitu kinakwenda sawa. Maandalizi karibu yote yamekamilika...ni #UKAWA Julai 14.

Hilo ndilo suala la msingi kwa sasa. Baada ya giza totoro la siasa za ghiliba, rushwa na hila huko Dodoma kwa takriban mwezi mzima, wananchi wanasubiri nuru ionekane Julai 14 kupitia UKAWA. Yamebakia masaa mchache kuuona mwanga unaosubiriwa na Watanzania wote wapenda mabadiliko ya kimfumo na kiutawala, si mabadiliko ya majina na sura za watu kutoka mfumo ule ule uliotukwamisha hapa tulipo.

Makene

Msako mkali Mexico wa muuza mihadarati


Mamlaka ya nchini Mexico limeanza msako mkali wa kumtafuta Joaguin Guzman gwiji la biashara ya madawa ya kulevya duniani, kufuatia kutoroka kwake katika gereza lenye ulinzi mkali mwishoni mwa wiki.
Helikopta za Blackhawk ambazo zimeonekana kuruka juu gerezani Altiplano magharibi ya Mexico City mahali alipokuwa ameshikiliwa huku ndege zote zikiwa zimezuiwa kuruka karibu na Uwanja wa ndege.
Wafanyakazi wa magereza wanahojiwa baada kubainika kuwa Joaguin alitoroka kupitia njia ya nchini ya ardhi yenye urefu wa kilomita moja na hii ni mara ya pili kutoroka.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Marekani, Loretta Lynch, ametoa msaada wa kumkamata Guzman ambae pia hujulikana kama ' El Chapo ' .

Van Persie atua Uturuki



Mashabiki wa manchester United wengi walijua kuwa Van Persie anaondoka kuelekea Fenabashe lakini kwa mtoto mdogo mwingereza wa miaka minne Louis Diamond hakufahamu kuwa kipenzi chake Robin Van Persie anaondoka mpaka pale alipoambiwa na wazazi wake kwamba mpachika magoli Robin alikuwa tayari kuelekea uturuki. Hivi sasa waturuki wameanzisha kampeni ya kuchangishana pesa ili mtoto huyo ambaye video yake imesambaa mitandaoni na kutizamwa na watu wengi aletwe Uturuki kumshuhudia mchezaji huyo.
Shabiki huyo mdogo wa miaka minne alipoambiwa na wazazi wake kuwa Van Persie alirekodiwa na baba yake akilia sana na video yake imesambaa mitandaoni duniani kote.
"hatujamwambia kama video yake imesambaa duniani, tumemwambia tu kuwa tumewaonyesha marafiki zake tu hapa mtaani tu hajui kama ni dunia nzima, mimi na mke wangu tuna hamu ya kumwona atakavyocheka tukimwonyesha video hii miaka kumi baadaye" Alisema baba wa mtoto huyo.
Kuna uwezekano pesa iliyopangwa kuchangwa mashabiki wa uturuki ikazidi kiwango cha pauni 1200 za uingereza kilichokusudiwa kumsafirisha mtoto huyo na baba yake ili kuja kushuhudia mechi ya kwanza ya Van Persie nchini uturuki.
Ni vema pia mtoto akapozwa kwa kuambiwa kuwa kinakuja chuma kipya kutoka southampton, Morgan Shineidelini ambaye atafanya vipimo Man U.
Kwa upande mwingine Liverpool inachukua kitita cha pauni milioni 49 kumuuza Raheem Sterlin kuelekea Man City na kumfanya kijana huyo mdogo wa miaka 20 kuwa mchezaji wa ghali zaidi katika england.