Arsenal kumnunua Wanyama na Mitrovic
 
 
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger 
anapanga kumnunua kiungo wa kati wa Southampton Mkenya Victor Wanyama na
 mshambuliaji wa Anderlecht Aleksandr Mitrovic kulingana na gazeti la 
the Sun nchini Uingereza.
Wenger amejiandaa kutoa kitita cha pauni
 millioni 30 kwa wachezaji hao wawili,huku Wanyama akigharimu kitita cha
 pauni millioni 20 naye mshambuliaji huyo wa Anderlecht Mitrovic 
akigharimu pauni millioni 10.
Inaaminika kuwa Wanyama ataondoka 
katika kilabu ya Southampton iwapo atachukuliwa na kilabu kikubwa huku 
naye Mitrovic akiwa amekuwa akifuatiliwa na waajiri wa Arsenal katika 
kipindi cha wiki chache zilizopotea.
Mitrovic amekuwa akifananishwa na Didier Drogba kutokana na mchezo wake.
Credits:BBC 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment