Rais Nkurunzinza wa Burundi amfuta kazi msemaji wake mkuu
 
Kufuatia joto 
la kisiasa ambalo limeendela kupanda nchini Burundi, huku chama tawala 
Cndd- Edd kikikumbwa na mgawanyiko, rais Pierre Nkurunziza, amemfuta 
kazi msemaji wake, Léonidas Hatungimana.
Wakati huohuo, Pierre Nkurunziza amewateua wasemaji wake wapya, ikiwa ni
 pamoja na msemaji wake mkuu, Gervais Habayeho pamoja na naibu msemaji 
wake Louis Kamwenubusa, aliyekua mkurugenzi wa redio inayomilikiwa na 
chama cha Cndd-Fdd, Rema Fm. Mkurugenzi mkuu wa redio na televisheni vya
 serikali (Rtnb), Thadée Siryuyumunsi amefutwa kazi, na nafasi yake, 
ameteuliwa Jérôme Nzokirantevye, aliyekuwa msemaji wa spika wa Bunge.
Sakata hilo lakuwafuta kazi baadhi ya vigogo katika taasisi mbalimbali 
za nchi linakuja baada ya vigogo hao wakiwa pia wafuasi wenye ushawishi 
mkubwa katika chama tawala Cndd-Fdd kutia saini kwenye waraka unaomtaka 
rais Pierre Nkurunziza kutogombea muhula wa tatu katika uchaguzi ujao wa
 urais.
Hata hivyo wafuasi hao wa chama tawala wameapa kutotetereka na uamzi huo
 wa kuwafuta kazi, huku wakibaini kwamba wataendelea na msimamo wao hadi
 pale rais Nkurunziza atakubali kusitisha nia yake ya kugombea muhula wa
 tatu katika uchaguzi wa urais unaopangwa kufanyika mwezi Juni.
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment