 PROFESA
 Mwesiga Baregu
PROFESA
 Mwesiga Baregu, mmoja wa watu wanaoheshimika nchini amesema, aliyepata 
kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, anaponzwa na 
kibuli cha kujiona hakuna zaidi ya yeye.
 
         PROFESA
 Mwesiga Baregu
PROFESA
 Mwesiga Baregu, mmoja wa watu wanaoheshimika nchini amesema, aliyepata 
kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, anaponzwa na 
kibuli cha kujiona hakuna zaidi ya yeye. 
Amesema, Zitto ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa
 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tanzania Bara na naibu 
kiongozi wa upinzani bungeni, anafanya kazi asiyoifahamu na ambayo haina
 mavuno.
“Ninamfahamu
 vizuri. Wakati tuhuma hizi za usaliti zilipoanza kuibuka, Kamati Kuu 
ilinikabidhi jukumu la kumsaidia mama yake mzazi kumlea kijana huyu.” 
Kauli ya Baregu ilitolewa siku moja baada ya Zitto kujiondoa bungeni na baadaye kujiunga na Chama cha ACT – Tanzania.
Prof. Baregu aliwahi kuwa “mlezi wa Zitto” ndani 
ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Alikabidhiwa jukumu hilo
 na Shida Salum, mama mzazi wa Zitto (marehemu), baada ya mama huyo 
kuiomba Kamati Kuu (CC) ya chama hicho “kusaidia kumlea.”
Prof. Baregu ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya 
Chadema anasema, “Zitto hamnazo. Amekuwa anajiona yeye ni zaidi ya 
chama. Hashauriki.”
Anasema wakati ule alipopewa kazi ya kumlea Zitto 
“katikakati ya migogoro, tulikuwa tunazungumza naye mara kwa mara. 
Ninamfahamu. Kazi hii ya kumlea tulikabidhiwa mimi na mama yake mzazi, 
Bi. Shida Salum,” anaeleza Baregu.
Mama mzazi wa Zitto, alifariki dunia Juni mwaka jana, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kauli ya Prof. Baregu ilifuatia gazeti hili kutaka
 maoni yake juu ya mustakabali wa kisiasa wa Zitto baada ya kuwahi 
kujiondoa ndani ya Chadema.