Waangalizi wa UN Burundi wamefuatilia uchaguzi
    
 
Uchaguzi wa Bunge na serikali za mitaa ulifanyika jana 
nchini Burundi, licha ya shinikizo la jamii ya kimataifa la kutaka 
uahirishwe kutokana na mazingira ya kisiasa na kiusalama.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kufuatilia uchaguzi nchini 
Burundi, MENUB umesema waangalizi wake 36 wamefanikiwa kufuatilia 
uchaguzi bila kutishiwa usalama wao.
 Msemaji wa MENUB Vladimir 
Monteiro, akihojiwa jana, alisema waangalizi wa MENUB wametembea kwenye 
majimbo yote ya Burundi ili kufuatilia utaratibu huo na kuandaa ripoti 
kwa ajili ya Katibu Mkuu na Baraza la Usalama. 
Serikali ya Burundi ilishikilia msimamo wake wa kufanya 
uchaguzi jana tarehe 29 Juni, kinyume na mapendekezo ya timu ya 
uhamasishaji iliyohusisha Umoja wa Mataifa na mashirika ya kikanda, ya 
kuhairisha uchaguzi hadi Julai, tarehe 30.
Monteiro ameeleza msimamo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa 
Mataifa Ban Ki-moon kuhusu uamuzi huo.Ameongeza kuwa Katibu Mkuu 
amesikitishwa kwamba mapendekezo ya timu ya uhamasishaji kuhusu 
kuhairishwa kwa uchaguzi hayakusikilizwa, lakini kwamba anaendelea 
kuwaomba wadau wa Burundi waendelee kufanya kazi ili kupata suluhu 
kupitia mazungumzo, bila ghasia.
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment